Thursday 13 March 2014

UTAGUNDUAJE KAMA UNA MIMBA CHANGA?

Mara nyingi ni vigumu mwanamke kugundua kama ameshika mimba siku za mwanzoni hadi pale anapokosa kuona siku zake za hedhi. pamoja na ugumu huo kuna dalili ambazo zinaweza kufanya uhisi kama una mimba katika siku za mwanzoni ambazo ni kuanzia  siku ya 18 toka mimba itungwe.

Dalili hizi zinatofautiana kwa kila mtu, wapo ambao wanaweza kuzipata zote na ambao hupata baadhi tu ya dalili hizi na pia wapo ambao hawazipati kabisa.

Miongoni mwa dalili hizo ni pamoja na:

1.JOTO LA MWILI KUPANDA.(basal body temperature stay high)

   Wanawake wengi hushindwa kutambua dalili hii pale wanapoipata kutokana na kutokuwa na uelewa
    juu ya miili yao.
    Hali hii inaonekana katika siku za mwanzo ambambo huweza kudumu kwa muda mrefu kiasi hivyo
    kama itadumu zaidi ya siku 18 basi ni vizuri kupima ili kujua kama inatokana na ujauzito au la.

2. KUPATA HAJA NDOGO MARA KWA MARA.(frequent urination)
    Kubanwa na haja ndogo mara kwa mara pia inaweza ikawa ni dalili mojawapo ya kuwa na mimba
    changa.

3.KUWA MWEPESI KUHISI HARAFU YA VITU  MBALI MBALI HASA  HARUFU MBAYA.(sensitivity to odors)
   Wakati wa mimba changa wanawake wengi wanakuwa wepesi wa kuhisi harufu ya vitu mbali mbali hasa zile harufu zisizo za kupendeza na kumfanya achukie vitu vingi vyenye kutoa harufu hizo.
 wakati kama huu si ajabu ukaona mtu hataki mume wake amsogelee kwa kudai anatoa harufu mbaya.
ukiona dalili kama hii inaweza ikawa ni ishara ya kuwa mjamzito hivyo unapaswa kufanya uchunguzi.

4.KUKOSA HEDHI.(missed period)
  Kwa kawaida mama mjamzito hapati siku zake za hedhi isipokua anaweza akapatwa na hali ya kuvuja kunakofanana na ile ya hedhi ila damu yake huwa nyepesi sana na hudumu kwa muda mfupi kati ya siku1 au 2 (implantation bleeding) hivyo    unapokosa kuona siku zako za hedhi
  unapaswa kuchunguza sababu za kukosekana kwa hedhi.

5. KICHEFU CHEFU AU KUTAPIKA.( Nausea or vomiting)

Thursday 27 February 2014

HUMAN PAPILOMA VIRUS INFECTION.

Ugonjwa huu husababishwa na kirusi aitwaye HPV(Human Papiloma Virus), kuna aina 90 za kirusi huyu lakini aina 4 ndio huonekana mara kwa mara(HPV-6, HPV-11, HPV-16 na HPV-18)
Mara nyingi husababisha viotezo mfano kwenye picha inaweza kua kimoja au vingi mfano hapo kwenye picha, hutokea sehemu za haja ndogo, kubwa na sehemu za uzazi(uke, uume, mfuko wa uzazi)
Dalili huonekana kuanzia miezi 3 mpaka miaka 2 baada ya maambukizi

Kuzaa


Vifo vya akina mama wakiwa na Mimba Vinapungua!
Utafiti wa mwaka 2010 wa Hali ya Afya ya Jamii  (UHAJ)  waonyesha mafanikio huduma za Uzazi
Utafiti wa Hali ya Afya ya Jamii 2010 (UHAJ) au kwa Kizungu DHS unaonyesha mafanikio makubwa hasa katika nyanja nne: mahudhurio  ya kliniki wakati wa kujifungua, kujifungulia hospitali, kujifungua ukisaidiwa na mhudumu wa afya yaani nesi au daktari na kupunguza vifo vya akina mama wenye mimba na wakati wa kujifungua
Kuhudhuria kliniki ya uzazi  na kupima mimba ni huduma muhimu ambapo wafanyakazi wa afya, manesi na madaktari wanampima mama na kumfuatilia ili kuyazuia matatizo yanayojitokeza wakati wa mimba, kuyatambua na kuyatibu mapema.  Kwa kupima na kufuatilia mimba kutoka inapotungwa mpaka mtoto anapozaliwa kunazuia na kupunguza matatizo yanayoweza kutokea kwa mama na mtoto wakati wa mimba, wakati wa kujifungua na baada ya kujifungua.
Hapa kwetu Tanzania karibu akina mama wote wenye mimba, kiwango cha tisini na sita kwa mia (96%) hupimwa mimba yaani huhudhuria kliniki ya kina mama wenye mimba angalau mara moja wakati wakiwa na mimba. Utafiti wa Hali ya Afya  ya Jamii (UHAJ) wa   2004-05;  kiwango hiki kilikuwa tisini na nne kwa mia (94%) kwa hiyo UHAJ wa mwaka 2010  umeonyesha ongezeko kidogo  la  mbili kwa mia (2%). Ni vizuri kuona kuwa kuhudhuria kliniki wakati wa mimba ni moja ya huduma ambazo akina mama wana mwamko sana nazo wawe wa kijijini au wa mjini; wenye uwezo kiuchumi au wasio na uwezo wa kiuchumi,  wenye uwezo sana au wenye uwezo hafifu; wote huhudhuria kliniki wakati wakiwa na mimba
Mimba ya miezi saba
Usafi wakati wa kujifungua
Kujifungua kwenye hali ya usafi na pahala ambapo kuna huduma ya daktari au nesi kunapunguza sana uwezekano wa kupata matatizo wakati wa kujifungua yaani matatizo kwa mama na kwa mtoto. Inapunguza sana uwezekano wa kudhurika mama au mtoto. Mama akijifungulia nyumbani, akijifungulia mahali ambapo siyo pasafi; panapokosekana vifaa muhimu na wataalamu yaani daktari au nesi; mama na mtoto wana uwezekano wa kupata madhara ya kuumia na kupata maambukizi ya bakteria, virusi au fangasi.
Nusu ya mama wanaojifungua Tanzania yaani hamsini kwa mia (50%) huzalia kwenye kituo cha huduma za afya yaani hospitali, kituo cha afya au zahanati. Nusu yaani 50% huzalia  nyumbani. Hii tena ni ongezeko kutoka  UHAJ wa  2004-05 ulioonyesha kuwa arobaini na sita kwa mia (46%) ya akina mama wenye mimba  walikuwa wanazalia hospitali na 54% walikuwa wanazalia nyumbani.
Huyu mtoto amezaliwa sasa hivi
Kuna tofauti kati ya akina mama wanaozalia nyumbani na wale wanaozalia hospitali. Akina mama vijana yaani walio na mimba za mwanzo na wale wanaoishi mijini wanatumia huduma za kuzalia hospitali zaidi kuliko wale wanaojifungua mimba za baadaye, walio na umri mkubwa na wanaoishi vijijini. Inavyoonekana ni kuwa akina mama wakishaendelea kujifungua basi hupunguza kuzalia hospitali na badala yake hujifungulia nyumbani.
Akina mama wenye elimu kwa mfano wale ambao wamesoma mpaka sekondari na vyuo vikuu wana uwezekano wa mara mbili wa kujifungulia hospitali na kujifungua huko wakisaidiwa na daktari au nesi kuliko akina mama ambao hawana elimu.
Vifo vya kina mama wakati wa mimba na kujifungua
Vifo vya kina mama vinavyohusiana na uzazi ni vifo vinavyotokea wakati wa mimba, wakati wa kujifungua au miezi miwili baada ya kujifungua.
UHAJ wa 2010 ilionyesha kuwa vifo vya kina mama wakati wa mimba au kujifungua ni kiasi cha kumi na saba kwa mia (17%) ya vifo vyote vya kina mama wa miaka (15-49).  Riski ya kupoteza maisha wakati wa mimba na kujifungua ni 0.8 kwa kila akina mama 1,000
Vifo vya kinamama wakati wa kujifungua au kwa lugha ya kitaalamu ‘Maternal Mortality Ratio’ ni vifo 454 kwa kila wanawake laki moja (100,000) wanaojifungua watoto hai. Turahisishe hii takwimu kwa kusema kuwa katika wanawake 2,000 wanaojifungua watoto hai mwanamke mmoja hufariki. Kiwango hiki cha 454/100,000 ni pungufu ya kiwango kilichoonekana kwenye UHAJ wa 2004-05 ulioonyesha takwimu ya 578/100,000 na ya 1996 iliyoonyesha 529/100,000
Kama unavyoona takwimu hii na namba ya akina mama wanaokufa wakati wa mimba na kujifungua ilionyesha kuongezeka kutoka 529/100,000 mwaka wa 1996 na kuongezeka mpaka 578/100,000 mwaka wa 2004/05 na sasa mwaka wa 2010 imepungua kufikia 454 /100,000. Kwa hiyo imepungua hata kupitiliza na kuwa chini zaidi ya mwaka  1996 ilipokuwa  529/100,000. Kupungua  kwa takwimu hii ya  idadi ya vifo vya akina mama wenye mimba na wanaojifungua ni ishara nzuri kuwa jitihada zinazofanyika kupunguza vifo vya kina mama na watoto wachanga zinaanza kufanikiwa. Pamoja na kupungua idadi hii bado iko juu sana na haivumiliki. Kifo cha mzazi, hata kikiwa kimoja hakivumiliki. Ni muhimu kuziendeleza na kuzifikisha kwa wanaozihitaji hasa kwa wale wanaoishi vijijini.

Washkaji:
Mshikaji 1: Unajua mke wangu; hii ni mimba ya tatu na anasema eti atajifungulia nyumbani. Alizalia hospitali mimba ya kwanza na hakukuwa na matatizo. Na ya pili vile vile wala hakukuwa na matatizo. Sasa anasema maana hakuna matatizo basi hii atazalia nyumbani
Mshikaji 2: Duu! Kumbe ule utafiti wa UHAJ unavyosema ni kweli kabisa kuwa wanawake wanavyoendelea kuzaa ndivyo wanavyopunguza kuzalia hospitali. Kuzalia nyumbani ni jambo la hatari kabisa maana huwezi kujua matatizo yatakapojitokeza. Wanatuambia eti matatizo wakati wa mimba yanazidi kadiri mimba zinavyozidi kuwa nyingi kwa mama mmoja. Kumbe mojawapo ya sababu za akina mama kufariki wakati wa kujifungua ni kuwa wanapoona wamezalia hospitali na hakuna matatizo, basi mimba zinazofuata wanazalia nyumbani.
Mshikaji 1: Sasa nimkubalie azalie nyumbani au azalie hospitali? Wenzake, jinsi mimba zinavyozidi kuwa nyingi ndivyo hawazalii hospitali.
Mshikaji 1: Mpeleke akazalie hospitali maana hata ikitokea huko kuwa baada ya kujifungua umerudi nyumbani bila mke na mtoto au na mtoto bila mama hutalaumiwa lakini kama hayo yakitokea hapa nyumbani! Sijui

Maambukizi Yanayosambazwa kwa Kujamiana (MYKK)


Tunaelezea kwenye safu hii maambukizi yanayosambazwa kwa kujamiana. Wasomaji wengi wamezoea kuyaita magonjwa ya zinaa lakini habari hii inataka tubadilishe tuyaite ‘Maambukizi Yanayosambazwa kwa Kujamiana (MYKK)’ na tutaelezea kwa nini.
 Wanaojua Kizungu labda watakumbuka kuwa hapo awali tulikuwa tunaita hali hizi ‘Sexually Transmitted Diseases (STD). Ukitafsiri moja kwa moja maana yake ni Magonjwa Yanayoambukizwa Kujamiana . Tuliacha kuyaita STD na sasa tunayaita ‘Sexually Transmitted Infections’ (STI) yaani Maambukizi Yanayosambazwa kwa Kujamiana.
Kuna tofauti kati ya magonjwa (diseases) na maambukizi (infections) kwa kuwa magonjwa mengine yanasababishwa na maambukizi. Kwa hiyo tofauti kati ya magonjwa na maambukizi ni kuwa maambukizi yanazaa magonjwa. (Tofauti kati ya yai na kuku ni kwamba kuku anataga  yai).
‘Sexually Transmitted Infection’ (STI)  kwa Kiswahili cha moja kwa moja ni Maambukizi Yanayosambazwa kwa Kujamiana. Sexually transmitted Diseases (STD)  ni Magonjwa Yanayoambukizwa kwa Kujamiana. Utaona kuwa hapa  kuna tofauti kati ya magonjwa (diseases) na maambukizi (infections) Tatizo hapa siyo la ugonjwa tu bali ni la maambukizi. Kunaweza kukawa na maambukizi yanayotokana na  kujamiana ambayo unayaona  maambukizi yenyewe, yaani unaona wadudu ambao mtu ameambukizwa kwa kujamiana, lakini huoni ugonjwa wenyewe. Hii inatokea wa mfano mtu anapoambukizwa na chawa wakati wa kujamiana  (chawa wa mafuzi). Unawaona chawa wenyewe lakini huoni ugonjwa.
Kwenye  tatizo la UKIMWI mtu anaambukizwa  na VVU. Haya ni maambukizi. Ugonjwa hauonekani moja ka moja bali kinachoonekana ni syndroma (dalili nyingi nyingi) inayosababishwa na magonjwa tegemezi yanayouvamia mwili baada ya kinga ya mwili kupungua. Maambukizi mengine kwa mfano ya kisonono na kaswende; ugonjwa unaonekana. Kwa sababu hizi za kuwa kuna hali nyingine ambapo ugonjwa hauonekani moja kwa moja na kwa kuwa katika hali zote kuna maambukizi basi ikakubalika hali hizi ziitwe Maambukizi Yanayosambazwa kwa Kujamiana (Sexually Transimitted Infections - STI)  Magonjwa Yanayosambazwa kwa Kujamiana (Sexually Transimitted  Diseases - STD)
Ni  Maambukizi ya Sinaa (MYS) au ni Maambukizi Yanayosambazwa kwa Kujamiana (MYKK)?
Ni lazima tuwashukuru wataalamu wanaojitahidi kutafsiri maneno yetu ya kisayansi kuyaweka kwenye lugha ya Kiswahili. Tushukuru kuwa tafsiri zao nyingi ni sawa na rahisi kuzitumia lakini kuna tafsiri ambazo wao wametupa kianzio ili na sisi tufikirie tuone kama zinahitaji kuboreshwa. Moja ya tafsiri ambayo inahitaji kuboreshwa ni hii ya kuziita hali hizi magonjwa. Tumeishatoa sababu hapo juu na kuelezea kuwa tuziite hali hizi maambukizi na siyo magonjwa.
Ukimwi unamtesa sana mwathirika
Kwa hiyo tuseme ni Maambukizi ya Sinaa?  Sinaa linamaanyisha starehe. Ni kama tunasema kuwa Maambukizi Yanayosambazwa kwa Kujamiana yanatokana na  sinaa, yanatokana na starehe. Hapa tunakuwa kama tunasema kuwa haya ni maambukizi yanatokana na kustarehe bila hata kusema ni starehe gani - ya kunywa pombe, ya kutumia madawa ya kulevya, ya kucheza dansi na musiki - starehe zipo nyingi. Tuyaite Maambukizi Yanayosambazwa na Starehe ya Kujamiana?
Ni ukweli kuwa ukichukulia kujamiana kama starehe utapata Maambukizi Yanayosambazwa kwa Kujamiana. Yanapotokea kati ya wanandoa yanatokana na mwanandoa mmoja au wote wawili kutokuwa waaminifu na kuchukulia kujamiiana kama starehe.
Ni vizuri jina la hali inayohusiana na ugonjwa unapolisikia linakueleza mengi juu ya hali yenyewe na linakuambia hata namna ya kujikinga na hali hiyo. Hapa ukisikia maneno matatu ya jina la hali hii ‘Maambukizi Yanayoambukizwa kwa  Kujamiana’ tayari umeishajua kuwa haya ni maambukizi; kuwa mwenzako anakuambukiza au wewe unamwambukiza. Ukisikia yanayosambazwa unajua kuwa yanasambazwa na siyo kwamba yanaambukizwa tu. Ukisema yanasambazwa tayari umeishasema kuwa yanaenea haraka sana kutoka mtu  hadi mtu. Ukisikia kuwa maambukizi haya yanatokana na kujamiana unaanza kujisemea ‘nijichunge sana na kujamiana ovyo ovyo.’
Maambukizi Yanayosambazwa kwa Kujamiana (MYKK) ni mtu kwa  mtu;  yaani yanatoka kwa mtu  mmoja yanaenda kwa mtu mwingine.  Siyo kama ilivyo kwenye ugonjwa wa kwa mfano malaria ambao vijidudu hutoka kwa mtu mmoja; vinaingia kwa mbu na baadaye kwa binadamu. Siyo kama wa kichocho ambao vijidudu vinatoka kwa mtu vinaingia kwenye konokono na baadaye vinaingia kwa mtu tena. Wataalamu wanaita hali hii ya jinsi vijidudu vinatoka kwa mwanadamu na baadaye kumrudia tena ‘mzunguko wa maambukizi’ ambapo kuna hatua mbali mbali.
Kwanza kuna wadudu wenyewe kwa mfano wanaosababisha Maambukizi Yanayosambazwa kwa Kujamiana; kuna hifadhi ya hao wadudu kwa mfano hapa anayewahifadhi ni binadamu; halafu wadudu wanaingia kwa mtu mwingine na huyo mtu mwingine anawapeleka tena kwa mtu mwingine. Maambukizi Yanayosambazwa kwa Kujamiana ni ya moja kwa moja kutoka kwa mtu hadi kwa mtu mwingine. Maambukizi ya magonjwa mengine yana mzunguko mrefu zaidi ambapo kuna wadudu wa maambukizi, kuna hifadhi yao ambayo moja inaweza ikawa binadamu (malaria na kichocho) au mnyama (kichaa cha mbwa); wadudu wanatoka kwenye hifadhi wanaingia kwenye mnyama mwingine kama kwa mfano kichocho kinaingia kwenye konokono, kinatoka huko na kuingia kwa binadamu. Kwa kujua mzunguko huu wa vijidudu vya magonjwa inajulikana ni wapi tuingilie ili kuuthibiti ugonjwa wenyewe. Kwa kuwa inajulikana kuwa mzunguko wa Maambukizi Yanayosambazwa kwa Kujamiana ni mtu kwenda kwa mtu; na yanaambukiza kwa kujamiana, kuyakinga haya maambukizi kunahusu kuiangalia hali ya kujamiana na kuhakikisha mtu anajamiana na mwenzake ambaye hana uwezekano wa kuwa na hifadhi ya Maambukizi Yanayosambazwa kwa Kujamiana (MYKK). Kuna watu ambao wana uwezekano zaidi wa kuwa hifadhi ya wadudu wa MYKK.  Kujikinga na maambukizi haya ni vema kutojamiana nao. Hawa ni watu wanaojamiana na watu wengi kwa mfano malaya au hata watu wa kawaida tu mradi wewe mwenyewe umemwangalia na kujua tabia yake. Ukishajua kuwa huyu anajamiana na wanaume au wanawake wengi au zaidi ya mmoja unajua kuna uwezekano kuwa yeye ni hifadhi ya  MYKK.
Tumeelezea ni kwa nini maambukizi haya yaitwe Mambukizi Yanayosambazwa  kwa Kujamiana na siyo Magonjwa Yanayosambazwa wa Kujamiana (STD) au Magonjwa ya Sinaa. Tuyaite Maambukizi Yanayosambazwa kwa Kujamiana au kwa kizungu STI. Wiki ujayo tutataja na kuanza kuelezea aina 13 za MYKK

Thursday 5 December 2013

STRESS Vs ADDICTION

STRESS Vs ADDICTION
 
 
 
 
the stressful situation that is associated with increased intensity or persistence of distress—the greater the uncontrollability and unpredictability of the stressful situation, lower the sense of mastery or adaptability, and greater the magnitude of the stress response and risk for maladaptive behaviors such as drug addiction.

JE UNAFAHAMU FAIDA NA UMUHIMU WA TENDO LA NDOA KWA WANA NDOA...?? SOMA HAPA NIKUFAHAMISHE,,,,

Kuwepo na mapenzi ya dhati kati ya wanandoa hufanya mambo mengi kuwa rahisi na mepesi bila kujalisha ni kipindi cha furaha au majonzi; sababu inakuwa upo na mtu ambaye anakufanyia unafuu wa mhusika kuamini kuwa kila kitu hatimaye kitakuwa sawa mradi huyo mpenzi wako yupo karibu na wewe anakupenda na mnashirikiana vilivyo kwa kujaliana kwa misingi ya ‘Chake changu, changu chake’.  

Mapenzi na kufanya mapenzi baina ya wawili wapendanao hasa kama wameoana ni moja ya chachu ya ndoa ambayo husaidia kushikilia na kuimarisha ndoa hiyo endapo ikatumika vizuri na kwa wote kufurahia hasa kwa wale ambao hushirikiana katika kila kitu.

Siri ya kufurahia tendo la ndoa ni wanandoa wote kuridhika na utendaji wa mwenza wao hasa wakati wa tukio, kwa kujituma, kuwa mbunifu, kutaka na kufurahia tendo hilo. Ingawa ni kweli kwa nadra inaweza tokea mwenzako akawa na hamu na wewe usiwe nayo (ikitokea mara chache sana – hili linaeleweka, na linaweza kukubalika ila si kwa kuzoea na ikawa utamaduni; iwe kwa mwanaume ama mwanamke) . 

Izingatiwe kuwa, kufurahia tendo la ndoa haiji kirahisi rahisi… Mazingira ya kufurahia tendo hili muhimu ni lazima yajengwe na yaimarishwe mara kwa mara. Maana ni wazi kuwa uhai wa kila ambalo linatakiwa kuishi ni lazima litunzwe kwa umakini na kujali. Hivyo kufurahia tendo la ndoa pia hupaswa kuimarishwa kwa nilivyotaja hapo awali – Kupenda, kujituma, utundu, maarifa na Ubunifu. Na haya yote huwa rahisi sana ikiwa mwanandoa wako wampenda ama kumkubali, na kubwa kuliko ikiwa na yeye pia hujituma, ‘ni mtundu’ na ana maarifa pia. 

Hivi vitu (Kujituma, utundu, maarifa na ubunifu) haviji hivi hivi pia… Na ndio kwa misingi hiyo wanandoa hushauriwa kuzungumzia tendo la ndoa, kama haridhiki katika tendo, kitu kipi hupendi, kitu gani unapenda, wapi unapenda kuguswa, vipi unapenda kukunwa, na ni kitu gani ambacho kinakupandisha mzuka – huku wewe mwenzie ukiwa mtundu katika kuhakikisha unavumbua maeneo mengine ambayo hata yeye hakujua kuwa anaweza pata raha hiyo ambayo anaipata kwa wakati huo (TAHADHARI – Yapaswa kuwa na mipaka pia). 

Mnaweza msiwe kila mmoja si mtaalam kwa mwenzie mnapoanza mahusiano yenu ya mapenzi, ila inapaswa na ni jukumu la kila mmoja kuhakikisha ufundi huo unaongezeka kadri siku zinavyozidi kwenda kwa mwenza wake huyo na si kupungua. Izingatiwe pia kuwa, Kufanya mapenzi si lazima ukafanya kama vile ambavyo picha za ngono huonyesha ili kujua mnafurahia, msingi ni kutafuta rhyme ambayo huwafanya wote mfurahie tendo hilo la ndoa na kuwafanya kuwa na kiu juu ya mwenza wako pale unapokuwa umemkosa. 

Ndoa si kufanya tu Mapenzi ni zaidi ya hapo, ila mwisho wa siku kufanya Mapenzi ni muhimu mno kwa ustawi wa ndoa kati ya wanandoa. Ni suala ambalo kiharaka haraka linaweza chukuliwa kwa wepesi, ila mwisho wa siku lina faida sana. 


FAIDA YA TENDO LA NDOA KWA WANANDOA

Linajenga ukaribu zaidi kwa wanandoa 
Tokana na majukumu ya kifamilia ambayo yanaenda yakikua kwa kasi na kufanya baadhi ya wanandoa kutokuwa na wakati wa kuwa karibu zaidi kunakuwa na muda mchache kwa baadhi kubadilishana mawazo. Wanandoa wengine wamefaulu kwa kuhakikisha kila siku/au mara kadhaa kwa juma kujulishana habari zao wanapokuwa hawapo pamoja. Tendo la ndoa linaweza tumika kama wakati muafaka wa kila mmoja kutiririka na kuongea mambo mbalimbali na hata kupanga mipango yenu ya kimaisha. Hilo hutokea pale mnapokuwa mnataka kujianda, nusu fainali au baada ya mchezo kuisha tegemeana na mtiririko wenu upo vipi. 
Black-couple-in-bed 

Kumwelewa Mwenzi wako 
Tendo la ndoa lina lugha yake… Tendo hili haliishi tu katika kufurahia na kufika kileleni bali pia linasaidia kumwelewa na kumsoma mwenzi wako. Ndio maana ni vema sana kumjulia mwenza wako kitabia na mwenendo kwa kuhusisha tendo hilo. Ikiwa wenza mna tabia ya kushirikiana na kuhusishana katika masuala ya kila siku ni rahisi kutambua kuwa mwenza wako siku hiyo kachoka, kachukizwa (iwe na wewe ama mtu mwingine), ana mawazo, ana wasiwasi, hana raha n.k. 
Haijalishi kuwa mwenza wako yupo katika hali ipi wengi hujitahidi hilo lisiwe kikwazo kwa tendo la ndoa (hasa wanaume) – Hivyo ni rahisi kumjulia tokana na namna mnavyokuwa faragha kujua kuna jambo ama la. Ni wazi wakati mwingine kunaweza kuwa na jambo na mwenzi wako asikuhusishe, kupitia tendo la ndoa unaweza pata viashiria. 

Inasaidia wanandoa kupata Watoto 
Watoto wana raha yake katika ndoa, na wana nafasi kubwa sana katika kuweza kuimarisha ndoa, kuleta furaha katika familia, kuwajenga na kuwa komaza kama wazazi na pia kuwaunganisha zaidi wanandoa kama mwili mmoja. Si wote wamejaaliwa kupata watoto (my heart goes out to them) – ila ukweli ni kuwa mara nyingi hiki ni kipengele muhimu katika ndoa ambacho wanandoa wenyewe na jamii hutarajia kuwa muhimu kufanikisha ili ndoa ionekane kuwa ina mafanikio. Niongeze kuwa tumepishana kutafsiri mafanikio ni nini katika ndoa, ila wengi huwa na msimamo wa kuwa watoto ni muhimu katika ndoa. 
sex-in-marriage 

Kutatua ugomvi/mgogoro kati ya wenza 
Ugomvi haukwepeki hata kama mwapendana vipi (ingawa frequency ya ugomvi hupishana kati ya wanandoa). Tendo la ndoa linazungumza mambo mengi sana…. Kitendo cha kukutana kimwili na mwenza wako kwa namna moja wapo inakuwa ni akili na mwili wako kukubali kuwa umejitoa kwa mwenzi wako kwa wakati huo. Kuna makabila ambayo hata uwe umegombana vipi na mke/mume wako, ikitokea tu ukalala naye na kufanya tendo la ndoa haijalishi kosa lilikuwa ni lipi inachukuliwa limesamehewa na yapaswa kusahau na kusonga mbele. 

Kupunguza uchovu/Msongo wa mawazo 
Ndoa ni moja ya njia kwa baadhi kuweza kupunguza uchovu alio nao na kwa wengine hata msongo wa mawazo. Tendo likifanywa vema na kwa ustadi, huweza kumwondolea mwenzi wako uchovu au msongo wa mawazo kwa kiwango kikubwa. Unafuu huo utegemea lakini, wengine inakuwa tu unafuu wakati wa tendo hilo na hali wengine hupata nafuu ya muda mrefu.  Hivyo ikiwa mwenzi wako yupo katika hali hiyo katika kutafuta namna ya kuhakikisha anapata unafuu, unaweza tumia tendo la ndoa kama silaha ya kumrudisha mwenzi wako katika hali nzuri. 

Linajenga heshima ndani ya ndoa (hasa kwa wanaume) 
Hili linawezekana pande zote (mke na mume) mmelipa umuhimu wa pekee tendo la ndoa hadi mkiwa faragha wote hufurahia tendo hili hadi kuna wakati mwajihisi mpo mwili mmoja kama si ndani ya ngozi moja. Tunarudi palepale, kuwa ni muhimu ukampenda mtu wako, ukapenda hilo tendo, mengine yanafuata mkiwa faraghani. 

Linatumika kupata unachotaka/Kulaghai (hasa kwa wanawake) 
black-love 
Hili linategemea unalifanya kwa namna ipi… Ukilifanya kana kwamba ni hongo ya lazima na kuwa wamaanisha hutokubali kuwa faragha bila kutimiziwa kitu Fulani – Hapo inakuwa ni tatizo na ndio ulaghai wenyewe. Ila lifanywapo kwa upendo, utani wa kimapenzi, kwa kutoa maneno matamu na kubembembeleza, husaidia kuongeza ashiki kwa wapenzi (inaweza isiwe kwa wote) na huku pia ukifanikiwa kupata kile ambacho unataka mwenzio akiwa katika mood nzuri. 

kipanya-artwork 
Wapendwa nakaribisha mawazo, michango, maswali, na maoni toka kwenu

BAADA YA SHULE KUFUNGWA MWALIMU WA SEKONDARI AMUA KUUZA KAHAWA MTAANI...!!

    
Hivi ndivyo Mnyetishaji wetu alivyomnasa ticha huyu wa sekondari mkoani Dodoma akiuza kahawa mtaani ili kujinusuru na ukata wa maisha magumu ya kitaa, 

''Leta chikompe kyako nkupe kyai kya mata na kyai kya kapyaru...au kiguuju'' tcha jimmy:
  Pia mwalimu huyo pamoja na shughuli zote za uwalimu na kuuza kahawa pia na msanii anayefanya vizuri kwenye Game la music husasani mkoa wa Dodoma,



"Propaganda zinazoendelea sasa hivi zinatuimarisha CHADEMA"......Dk. Slaa

KATIBU Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Willibrod Slaa, amesema kamwe chama hicho hakitakubali kuwa legelege katika kusimamia misingi yake, ikiwemo katiba inayowaunganisha wanachama wote.

Alisema kuwa licha ya kuzushiwa propaganda nyingi ikiwemo udini na ukabila, lakini chama hicho kimefanikiwa kuzishinda hali aliyoelezea imewakomaza katika safari yao ya kuchukua madaraka.


Kauli hizo alizitoa jana mjini Kahama mkoani Shinyanga alipokuwa akihutubia mkutano wa hadhara katika viwanja vya CDT, ikiwa mwanzo wa ziara yake ya kukiimarisha chama.

Dk. Slaa alisema wakati wa kampeni za uchaguzi mkuu wa 2010, chama hicho kiliwaahidi Watanzania kuwa kama kingeshika dola, kingekuwa imara kusimamia serikali itakayowatumikia wananchi.

Alibainisha kuwa ili kuitimiza ahadi hiyo, chama hicho kamwe hakiwezi kuwa legelege kwa wanachama na viongozi wasiotaka kufuata katiba na taratibu za chama.

“Watanzania tulieni, tulieni, tulieni. Chama hiki kipo kwa ajili ya kuwatumikia ninyi na kusimamia maslahi yenu. Acheni ushabiki kwenye masuala mazito,” alisema.
Dk. Slaa alisema amekuwa akipigiwa simu na watu wengi wakimuulizia hali ya mambo inavyokwenda ndani ya chama hicho, hasa baada ya uamuzi wa Kamati Kuu kuwavua uongozi baadhi ya makada wake akiwemo mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe.

“Mimi nawaambia watulie tu… Nawaambia waviamini vikao vya chama chao, ndani ya CHADEMA hakuna mtu mkubwa kuliko katiba. Wote hapa tunaunganishwa na katiba.

“Chama hiki kimepita kila aina ya propaganda ikiwemo hii ya juzi ya ugaidi, zote tumezishinda na tutaendelea kuzishinda. Hata hii ya sasa inayosukumwa na mipango ya hujuma inayopangwa na CCM, wakishirikiana na vyombo vya dola na watendaji wa serikali, tunazidi kuimarika na kutukomaza kwenda kushika dola.

“Wakati wa kampeni mwaka 2010 tuliwaambia Watanzania kuwa tunakwenda kusimamia maslahi ya Watanzania. Tulisema elimu bure, mwaka jana wameamua kutuiga, tulisema vifaa vya ujenzi vishuke, pia wameamua kutuiga, lakini wameshindwa kutekeleza,” alisema.

Dk. Slaa alisema kuwa CCM wameshindwa kutekeleza kile kilichokuwa kikisemwa na CHADEMA, ambayo sasa inaamini ikiingia madarakani itatimiza mambo iliyowaahidi wananchi.
Safari yapata matatizo.

Ziara ya Dk. Slaa jana iliingia dosari baada ya magari aliyokuwa akiyatumia kupata hitilafu za kiufundi zilizosababishwa na kile kinachodaiwa ni mafuta machafu waliyoyaweka katika kituo kimoja cha mafuta kilichopo wilayani Kibaha mkoani Pwani.

Mafuta hayo yaliyafanya magari yaliyokuwa kwenye msafara huo kushindwa kwenda mwendo uliotarajiwa, na hivyo kusababisha Dk. Slaa na timu yake kufika katika viwanja vya mkutano saa 12 jioni.

Dk. Slaa leo anatarajia kwenda mkoani Kigoma ambako atahutubia mikutano mbalimbali ya hadhara pamoja na kufanya shughuli za kuimarisha chama kila eneo atakalolitembelea.

MIZENGO PINDA:MSHAHARA WANGU KAMA WAZIRI HAUZIDI SH MILION 6..

Waziri Mkuu amedai bungeni muda huu kwamba mshahara wake hauzidi Tsh. 6mil na akadai wanaodai analipwa zaidi ya hapo ni uzushi mkubwa kiasi kwamba yeye ni mkopaji tu katika mabenki na kuwa mshahara huo ni pamoja na mapato ya mkewe.

Source: Leo Bungeni -TBC


Saturday 30 November 2013

BENEFITS OF ONIONS

Never mind the tears they bring on—onions are an ace ally in your fight against disease. A prized member of the lily family, they lavish you with health benefits while adding oodles of taste to your food.
onions
A quick glimpse at their incredible health benefits:
  • The phytochemicals in onions improve the working of Vitamin C in the body, thus gifting you with improved immunity.
  • Onions contain chromium, which assists in regulating blood sugar.
  • For centuries, onions have been used to reduce inflammation and heal infections.
  • Do you enjoy sliced onions with your food? If yes, rejoice! Raw onion encourages the production of good cholesterol (HDL), thus keeping your heart healthy.
  • A powerful compound called quercetin in onions is known to play a significant role in preventing cancer.
  • Got bitten by a honeybee? Apply onion juice on the area for immediate relief from the pain and burning sensation.
  • Onions scavenge free radicals, thereby reducing your risk of developing gastric ulcers.
  • Those bright green tops of green onions are rich in Vitamin A, so do use them often.
My favorite way to enjoy onions is to slice them really thin, squeeze some lemon juice on top and add a little salt. Sprinkling a few freshly washed cilantro leaves adds fragrance and flavor to this simple, quick salad, without which no dinner of mine is complete

TAZAMA UZURI WA NYUKI ULIVYO

Baadhi ya wataalamu nchini wameanza kufanya utafiti juu ya tiba hii ya nyuki katika kutibu ‘gouts’. Waswahili wanasema, mtaka cha uvunguni sharti ainame. Pia wanasema, anayependa waridi, basi avumulie miiba. Vivyohivyo, hata katika tiba, wale wanaotaka uponyaji wamejikuta wakivumilia mambo mengi yanayoleta maumivu au kukera kama vile sindano na dawa. Hivyo, usishangae kuwa kuumwa na nyuki ikawa ni tiba tosha na thabiti kwako. Wanasayansi wa Chuo Kikuu cha Tiba cha Washington, Marekani wanaeleza kuwa, sumu ya nyuki inaweza kuponya maradhi mbalimbali ikiwamo kuharibu virusi vya Ukimwi bila kuharibu seli za mwili wa binadamu. Dk Joshua Hood, kiongozi wa utafiti huo anasema, ipo sumu kali iitwayo mellitin katika mwiba wa nyuki ambayo ina uwezo wa kuingia ndani ya mfuko unaozunguka kinga ya mwili wa binadamu na kuua virusi vya Ukimwi vilivyomo ndani.
Hata hivyo, imeelezwa kuwa sumu hiyo ya Mellitin iingiapo kwa wingi katika mwili wa binadamu, inaweza kuleta madhara.
Pia, Profesa Samule Wickline pia wa Marekani aliunda chembe ndogo zenye sumu ya mellitin, ambayo ina uwezo wa kuzuia saratani au dalili zozote z  vivimbe vya saratani.
Hapa nchini, Dk Augustine Godman mtaalamu wa magonjwa ya uzeeni na mshauri wa kisaikolojia anasema amejaribu kutumia tiba ya nyuki kwa wagonjwa 158 wenye matatizo kwenye viungio vya mwili (gouts), ambayo husababishwa na wingi wa tindikali ya uric katika damu.
Anasema dawa hiyo imeonyesha matokeo mazuri kwa wagonjwa wengi ambao hung’atwa na nyuki katika sehemu mbalimbali za miili yao. Dk Godman anasema, yeye humuweka mgonjwa nje ilipo mizinga ya nyuki na kisha kuwafungulia wadudu hao kutoka katika mizinga yao.
Anasema nyuki wana sumu ambayo inaingia katika mwili wa binadamu na kuondoa sumu iliyo mwilini.
Wakati huohuo, Dk Hood anasema kuwa, sumu ya nyuki ina uwezo mkubwa wa kutoa tiba na kuunda mafuta ya uke ambayo yanaweza kuzuia maambukizi ya VVU na kuviua virusi sugu.
Watafiti hao wanaeleza kuwa sumu ya nyuki ina uwezo wa kuua wale askari wakubwa wanaofanya mashambulizi katika kinga ya mwili.
nyuki
Profesa Ibadan Selako kutoka Chuo Kikuu cha Tiba Nigeria, anasema miba ya nyuki ndiyo silaha yao kuu wanayotumia wadudu hao kujilinda, kumlinda malkia na askari wengine, ni silaha ambayo ikitumiwa hata kwa binadamu inaweza kufanya maajabu.
“Mungu ameweka kitu cha ajabu katika sumu ya nyuki. Sumu hiyo inaweza kutibu mara tu nyuki anapokuuma na kuingiza miba yake katika mwili wako, baada ya dakika 45 au saa moja, nyuki hufa, na sumu aliyokuachia huingia katika mfumo wa mwili wako na kuanza kufanya maajabu,” anasema Profesa Selako.
Anasema, sumu ya nyuki inapoingia katika mwili wa mwanadamu husababisha maumivu na maumivu hayo pia huondoa maumivu. Salako anasema, ameshawahi kuwatibu watu wanaoishi na virusi vya Ukimwi na wengi wao wamepona kwa kutumia sumu hiyo ya nyuki.
Anasema mgonjwa huanza tiba ya kung’atwa na nyuki na huendelea na tiba hiyo kwa wiki nane hadi 12 kisha huenda kupimwa.
“Akienda kupima ataona kabisa kiwango cha virusi kwenye mwili wake kimepungua baada ya wiki nane hadi 12 za matibabu baada ya hapo tutaacha kumpa tiba, na kisha tutaendelea na tiba kwa wiki nyingine nne hadi tano, mgonjwa huenda kupima tena,” anasema
Profesa Selako anasema mgonjwa atakapokwenda kupima kwa mara ya pili, atagundua kuwa virusi katika mwili wake vinashuka kila anapoendelea na tiba na baadaye atakuta hana VVU. Anasema, nyuki wa kiume kwa kitaalamu huitwa ‘drone’ na hawana uwezo wa kutoa sumu kali kama nyuki wa kike ambao ndiyo malkia.
Shirika la Utafiti wa Ukimwi Duniani (FAIR) linasema duniani kote watu zaidi ya milioni 34 wanaishi na Virusi vya Ukimwi huku kati yao, 3.3 milioni wapo chini ya umri wa miaka 15. Wengine zaidi ya 7,000 hupata maambukizi mapya kila siku duniani.
Wakati huohuo, wanasayansi katika viwanda vya urembo duniani wamefanikiwa kutengeneza mafuta ya ngozi yenye sumu ya nyuki. Mafuta hayo ya ngozi huingia katika ngozi na kutoa sumu, kuirutubisha ngozi na kuondoa makunyanzi.
Mafuta hayo tayari yameshapata wateja  wengi, hasa baada ya Malkia Mtarajiwa, Kate Middleton kuyatumia kabla ya harusi yake na kuonyesha matokeo mazuri.
Kipodozi hicho kiitwacho Radial Bee Venom kina uwezo wa kuondoa ukavu usoni na makunyanzi na kinawasaidia zaidi watu wanaokaa katika jua kwa muda mrefu.
Dk Christopher Kim, Mkurugenzi  wa Taasisi ya Tiba ya Redbank anasema, tiba ya sumu ya nyuki iligunduliwa zaidi ya miaka 1,000 iliyopita na vielelezo vya tiba hiyo vinaonekana katika maandishi ya tiba za Ugiriki na Misri.
 Anasema tiba hiyo ilianza pindi wale wanaotunza nyuki walipoumwa mara kwa mara na wadudu hao kisha wakajisikia kupona baadhi ya maradhi kama maumivu ya kichwa, neva za fahamu, viungio vya mwili na kuwashwa.
 Kwa upande mwingine, zao la nyuki hawa yaani asali, ni tiba kwa vidonda, ngozi ya uso na huwasaidia watu wenye matatizo ya vidonda vya tumbo.
Dk Imelda Mwakitumbo wa Hospitali ya Mikocheni anasema asali ya nyuki hasa wadogo ina manufaa makubwa katika kuponya majeraha.
“Lakini pia mtu ambaye anataka kuondoa seli zilizokufa katika uso akipaka asali kwa maelekezo maalumu, anaweza kuipendezesha ngozi ya uso wake,” anasema Dk Mwakitumbo
Chanzo:Mwananch

Friday 29 November 2013

DAWA YA MAFUA ISIYO NA MADHARA

Watu wengi husumbuliwa sana na mafua makali na wakati mwingine kupiga chafya mfululizo. Ili kuondokana na tatizo la mafua unashauriwa kuandaa kinywaji kifuatacho kisicho na kemikali :
MAANDALIZI
Chukua :
1. Maji lita moja
2. Asali vijiko 3 vikubwa vya chakula
3. Tangawizi ya unga kijiko kimoja kikubwa cha chakula au tangawizi mbichi itwange upate mchanganyiko uliopondeka kijiko kimoja kilichojaa.
Chemsha mchangyanyiko wako wote huo kwa pamoja mpaka uchemke vizuri ambapo inategemea na moto wa jiko lako lakini mpaka utakapoona imechemka vizuri usiache ikakaukia jikoni inashauriwa dakika 15 hadi 20 inatosha.
Kisha iache ipoe na KUNYWA NUSU GLASI MARA TATU kwa siku yaani asubuhi , mchana na usiku.
mafua
Kwa wale walio na mafua sugu yanadondoka muda wote na kupiga chafya nyingi sana zisizo na idadi basi zitakata mara moja na siku ya pili zitaisha kabisa kumbuka kunywa dawa hii mwezi mzima au hadi miezi miwili utapona kabisa.
Kinywaji hiki ni dawa ya mafua safi kabisa unatumia siku moja tu unakua na nafuu kabisa ila dozi yake inataka utumie mwezi mmoja hadi mwezi mmoja na nusu mfululizo bila ya kuacha.

AFYA JE..?? FAHAMU KIUNDANI UGONJWA WA PUMU (ASTHMA) NA DALILI ZAKE...

Utangulizi Ugonjwa wa pumu ni ugonjwa sugu ambao huathiri njia za hewa ambazo huingiza na kutoa hewa katika mapafu. Upatapo ugonjwa wa pumu, kuta za ndani za njia ya hewa hupata maumivu (inflammation) na kuvimba. 

Maumivu katika njia za hewa huzifanya kujihami kwa kusinyaa na hivyo kupunguza kiasi cha hewa kinachopita kwenda kwenye mapafu. Hali hii husababisha muathirika kutoa mlio kama wa filimbi au mluzi wakati wa kupumua. 




Pumu husababishwa na nini? 

Bila shaka mpenzi msomaji umekua ukijiuliza swali hili mara kwa mara. Haifahamiki haswa ni sababu zipi zinazopelekea njia za hewa kupata maumivu na hivyo kupelekea mtu kupata pumu. 

Vyanzo mbali mbali vinaonyesha kuwa inatokana na mseto wa vitu kama tumbaku, maradhi na baadhi ya vizio

Pia kuna vitu katika mazingira ambavyo vinaweza kusababisha mtu kushambuliwa na pumu. Vitu kama vile mazoezi, vizio, viwasho (irritants) na maradhi yatokanayo na virusi. 

Baadhi ya vizio ni kama vifuatavyo: 

-Vumbi 
-Mende 
-Chavua (pollen) kutoka kwenye miti na majani 
-Magamba ya wanyama, manyoya n.k 

Viwasho kama: 
-Moshi wa sigara 
-Uchafuzi wa hewa 
-Harufu kali (kutoka kwenye rangi au chakula) 
-Msongo wa mawazo 
-Dawa kama Aspirin 
-Ugonjwa wa kucheua 
-Viwasho au vizio vitokanavyo na kemikali 
-Magonjwa ya njia ya hewa n.k.

Ieleweke kwamba orodha iliyotajwa hapo juu siyo kamilifu kwa maana kwamba haijasheheni vitu vyote vinavyoweza kuleta dalili za pumu na pia muathirika anaweza kuathirika na kimoja wapo au zaidi. 

Vigezo hatarishi 

Baadhi ya vigezo hatarishi vinavyoweza kuongeza uwezekano wa kusababisha ugonjwa wa pumu ni pamoja na: 

-Kuishi katika miji mikubwa, haswa katikati ya mji ambapo huongeza uwezekano wa kukutana na vizio 

-Kuvuta hewa iliyo na moshi 

-Kemikali zitokanazo na kilimo, dawa za kutengeneza nywele, rangi, vyuma, plastiki au vifaa vya elektroniki 

-Kuwa na mzazi mmoja au wawili wenye pumu 
-Kuathirika na maradhi ya mfumo wa hewa kama kikohozi na mafua wakati wa utoto. 

-Unene wa kupita kiasi (obesity) 

-Ugonjwa wa kucheua na kiungulia (Gastro esophageal reflux disease) 

Dalili za Pumu 

Baadhi ya dalili za kawaida za ugonjwa wa pumu ni kama zifuatazo: 

-Kikohozi: Mara nyingi kikohozi cha pumu huwa kikali nyakati za usiku au alfajiri na hivyo kumfanya mwathirika kutolala vizuri 

-Kutoa sauti ya mfano wa mtu anayepiga mluzi au filimbi wakati wa kupumua 

-Kifua kubana: Mgonjwa husikia kama kitu kinakandamiza kifuani au wakati mwingine husikia kama mtu amemkalia kifuani. 

-Kukosa hewa: Baadhi hujisikia kama hawawezi kupumua na kukosa hewa ya kutosha inayoingia au kutoka kwenye mapafu. 

-Kupumua haraka haraka 

Ikumbukwe kwamba si watu wote huwa na dalili zilizokwisha tajwa hapo juu na dalili zaweza kutofautiana kati ya mtu na mtu. 

Dalili pia zinatofautiana ukali. Wakati kwa mwingine dalili zinakuwa za wastani, wengine zinakuwa za kukera tu au mbaya kiasi cha kumzuia muathirika kufanya shughuli zake za kila siku. 

Vile vile wapo wengine ambao dalili zinakuwa mbaya kiasi cha kuhatarisha maisha. Dalili pia zaweza kutofautiana kwa kipindi zinapotokea. 

Wengine hupata dalili mara moja tu kwa mwezi, wengine kila wiki na wengine hupata dalili kila siku. Hata hivyo iwapo muathirika atapata matibabu sahihi anaweza kuishi na dalili chache au bila dalili kabisa


AFYA JE...?? UNAFAHAMU FAIDA ZA KULA MBEGU ZA MABOGA....?? SOMA HAPA NIKUJUZE...

Unaweza kuzidharau mbegu za maboga, lakini ni miongoni mwa mbegu zenye faida kubwa mwilini, zinazoweza kuzuia na kutibu hata magonjwa hatari yaliyoshindikana hospitalini.

 
Kwa mujibu wa utafiti wa kisayansi uliokwishafanyika, zifuatazo ni faida za kifya mtu anazoweza kuzipata kwa kula mbegu za maboga, zikiwa mbichi ama zilizokaangwa:

HUIMARISHA MOYO, MIFUPA
Mbegu za Maboga (Pumkin Seeds), zina kiwango kingi cha madini aina ya Magnesium ambayo ni muhimu kwa afya ya moyo, uimarishaji mifupa, mishipa ya damu na ufanisi wa utumbo mpana. Magnesium imeonesha uwezo mkubwa wa kuzuia mshituko wa moyo na kiharusi.

KINGA YA MWILI
Mbegu za maboga zina kiwango kingi cha madini aina ya Zinc, ambayo yana faida nyingi mwilini, zikiwemo uimarishaji wa kinga mwilini, ukuaji wa seli, macho na ngozi ya mwili. Vile vile Zinc huimarisha nguvu za kiume.

SARATANI YA KIBOFU
Kutokana na kuwa na kiwango kingi cha Zinc, utafiti umeonesha kuwa mafuta na mbegu zenyewe za mabogo huweza kutumika kama dawa ya kutibu saratani ya kibofu.

KINGA YA KISUKARI
Utafiti umeonesha pia kuwa mbegu za maboga huweza kuimarisha utokaji wa ‘insulin’ mwilini, hivyo kuwa kinga au kuleta ahueni kubwa kwa wagonjwa wa kisukari.

TIBA KWA WALIOFIKIA UKOMO
Mafuta ya mbegu za maboga hayana madhara, zaidi yana kirutubisho muhimu cha kurekebisha Cholesterol mwilini, kushusha shinikizo la damu, kuzuia uvimbe, maumivu ya kichwa, maumivu ya viungo vya mwili na vile vile huondoa maumivu mbalimbali yanayowapata wanawake wenye umri mkubwa waliofikia ukomo wa hedhi (Menopause).

UGONJWA WA INI
Mbegu za maboga pia zina kamba lishe na kinga kubwa ya kupambana na magonjwa nyemelezi. Mbali na hayo, mbegu zina virutubisho vinavyotoa kinga dhidi ya magonjwa ya ini na moyo.

USINGIZI
Kwa watu wenye matatizo ya usingizi, wanashauriwa kula punje kadhaa pamoja na tunda lolote muda mfupi kabla ya kupanda kitandani, utafiti umeonesha kuwa mbegu za maboga zina kirutubisho kinachochea uzalishaji wa homoni za usingizi kwa wingi.

UVIMBE
Mbegu za maboga zimeonesha kuwa na virutubisho vingi vyenye uwezo wa kuzuia magonjwa yote ya uvimbe mwilini, yakiwemo ya kuvimba miguu, vidole na hata majipu.

JINSI YA KULA MBEGU
Hakikisha unakula mbegu ambazo hazijaoza na zilizosafi ambazo hazijakaa muda mrefu. Kwa usalama zaidi, zioshe kwa maji safi kisha zianike, inapendeza zaidi ukila bila kukaanga, lakini pia ukiamua kula za kukaanga bado utapata faida zake, muhimu usiziunguze wakati wa kukaanga. Kwa kawaida hukaangwa kwa muda usiozidi dakika 10 tu.


KWA WANAWAKE: FAHAMU DALILI KUMI ZA AWALI ZA KUGUNDUA KAMA UNA UJAUZITO (MIMBA)...




MWANAMKE anapopata ujauzito kwa kawaida huwa anaanza kuona dalili ambazo si za kawaida. Na ni wakati huo ambao ni muafaka kwake kuanza kuuchunguza mwili wake.Maumivu kwenye matiti:

Hii ni dalili ya kawaida ya ujauzito ambapo nguvu za homoni mwilini huongezeka wakati yai linavyopata “rutuba”, jambo ambalo huongeza wingi wa damu na kuyafanya matiti ya mwanamke kuvimba na kuwa makubwa isivyo kawaida.

Maumivu mwilini:

Utaanza kusikia maumivu kama vile unataka kuingia katika siku zako. Kwa kawaida hali hii hutokea wakati yai likiwa linasafiri kwenda katika chumba cha mimba. Hivyo, hali hiyo husababisha sehemu hiyo itanuke taratibu na kusababisha maumivu hayo.

Kutokwa damu bila kutegemea:


"Wanawake wengi hufikiria kutokwa na damu kidogo ni dalili ya kuwa katika siku zao. Lakini, katika hali halisi, kutokwa damu kusikotegemewa, huwakumba asilimia 25 ya wanawake wakati wa kurutubika kwa yai,” anasema Goist. Ambaye anaendelea kusema kwamba iwapo utaona hedhi yako inakuwa fupi au inafanyika katika hali ambayo si ya kawaida, unashauriwa kwenda kufanya kipimo cha ujauzito..

Kuchoka:


Unapojisikia kuchoka na kukosa raha, au kutaka hata kulala wakati ukiwa kazini, lazima ufahamu kwamba mwili wako unajirekebisha kuingia katika kipindi kipya cha mabadiliko.

“Tambua kwamba katika kipindi cha mwanzo cha ujauzito ni muda ambao mtoto tumboni huanza kutumia sehemu ya nguvu zako na hivyo kukuletea uchovu na usingizi” anasema Goist.

Chuchu kuwa nyeusi:


Chuchu huanza kubadilika rangi yake kutokana na chembechembe za uhai (seli) kuanza kufanya kazi kwa nguvu zaidi. Hata hivyo, Goist anasema: “Wanawake wenye ngozi nyeusi hawawezi kuiona dalili hii mapema hadi muda wa kama wiki kumi zipite.”

Kichefuchefu:


Hali hii huwapata asilimia 85 ya wanawake wanapopatwa na ujauzito, ambapo nyakati za asubuhi ndipo hasa hujionyesha. 

Mwili kuvimba:


Kuna wakati kupungua kwa nguvu za uyeyushaji chakula kunaweza kukusababishia kuona tumbo limevimba na nguo zikawa zinakubana kutokana na chakula kujaa katika utumbo. Lakini hali hiyo ikiendelea na ukaona siku zako haziji, basi ni vyema ukatambua kwamba tayari una ujauzito na kinachokupasa ni kwenda kuhakikisha.

Kwenda haja ndogo mara kwa mara:


Kwenda haja ndogo kila mara ni dalili kwamba kibofu chako kimeanza kufanya kazi ya ziada, ambapo huwa kinafanya kazi ya kuondoa maji kwa uthabiti zaidi wakati wa ujauzito. Hali hii pia hujitokeza mwishoni mwa ujauzito, ambapo kibofu kitakapokuwa kinarudia hali yake ya kawaida baada ya kufanya kazi kwa muda mrefu.

Tamaa ya vitu mbalimbali:

Kutokana na mwili kuwa na “mzigo” wa ujauzito na hivyo kuchoka, hali hiyo humfanya mwanamke kutamani vitu mbalimbali ili kukidhi mabadiliko yaliyojitokeza katika mwili wake. Hii ni pamoja na kutaka vyakula fulani au kufanya mambo ambayo hapo nyuma alikuwa hayapendi.

Kuumwa kichwa:

Kuongezeka kwa damu kunaweza kusababisha kichwa kuuma japokuwa si sana, hususani katika wiki za mwanzo za ujauzito. Hata hivyo, hali hii hukoma mwili unapojirekebisha na mzunguko wa homoni unaotokana na ujauzito.

Kufunga choo:


Homoni ambazo husababisha mwili kuvimba pia husababisha kufunga choo kutokana na mfumo wa kuyeyusha chakula kutofanya kazi vyema. Hata hivyo hali hii inaweza kujitokeza zaidi wakati ujauzito unapoendelea kukua.

Kuwa na hasira


"Kutokana na kuongezeka kwa homoni za utendaji kazi mwilini, hali hiyo itakusababishia uchovu, na kukufanya kuwa na hasira,” anasema Goist

Kuongezeka kwa joto mwilini:


Kipimo cha joto la mdomo ni muhimu katika kutambua hali ya ujauzito. Kwa kawaida joto huongezeka kwa nyuzi moja au zaidi wakati yai likiwa linatunga mimba. Hali hiyo ikiendelea kwa zaidi ya wiki mbili, itakuwa inaonyesha dhahiri kwamba kuna “mtoto anakuja”.


MMMHHH HII KALI...!! MAITI HUFUKULIWA MAKABURINI ILI KUBADILISHWA NGUO KATIKA KISIWA CHA SULAWESI HUKO INDONESIA..

Image

Image 

KILA mwaka huko kaitika kisiwa cha Sulawesi, Tana Toraja, Indonesia, wafu (au maiti) hufukuliwa kutoka makaburini ili kubadilishwa nguo na kuwatembeza kijini hapo. Watu wa eneo hilo wa kabila la Toraja wana mila ya ajabu inayoiitwa Ma’nene  ambayo wanaamini mtu akifa bado yuko nao kwa hiyo inawalizimu kufanya mambo hayo kama kuwabadilisha nguo.

Wao mtu akifa hutakiwa kuzikwa katika eneo alilozaliwa na si lazima azikwe katika eneo alilofia.
Idadi kubwa ya watu wa eneo hilo ni Wakristo, wanaofuata ni Waislam na wengine ni Wapagani ambao wanajulikana kwa imani au madhehebu ya Aluk To Dolo yaani “Njia ya Mababu”.
Wao mtu akifa hutakiwa kuzikwa katika eneo alilozaliwa na si lazima azikwe katika eneo alilofia.
Idadi kubwa ya watu wa eneo hilo ni Wakristo, wanaofuata ni Waislam na wengine ni Wapagani ambao wanajulikana kwa imani au madhehebu ya Aluk To Dolo yaani “Njia ya Mababu”