Saturday 30 November 2013

BENEFITS OF ONIONS

Never mind the tears they bring on—onions are an ace ally in your fight against disease. A prized member of the lily family, they lavish you with health benefits while adding oodles of taste to your food.
onions
A quick glimpse at their incredible health benefits:
  • The phytochemicals in onions improve the working of Vitamin C in the body, thus gifting you with improved immunity.
  • Onions contain chromium, which assists in regulating blood sugar.
  • For centuries, onions have been used to reduce inflammation and heal infections.
  • Do you enjoy sliced onions with your food? If yes, rejoice! Raw onion encourages the production of good cholesterol (HDL), thus keeping your heart healthy.
  • A powerful compound called quercetin in onions is known to play a significant role in preventing cancer.
  • Got bitten by a honeybee? Apply onion juice on the area for immediate relief from the pain and burning sensation.
  • Onions scavenge free radicals, thereby reducing your risk of developing gastric ulcers.
  • Those bright green tops of green onions are rich in Vitamin A, so do use them often.
My favorite way to enjoy onions is to slice them really thin, squeeze some lemon juice on top and add a little salt. Sprinkling a few freshly washed cilantro leaves adds fragrance and flavor to this simple, quick salad, without which no dinner of mine is complete

TAZAMA UZURI WA NYUKI ULIVYO

Baadhi ya wataalamu nchini wameanza kufanya utafiti juu ya tiba hii ya nyuki katika kutibu ‘gouts’. Waswahili wanasema, mtaka cha uvunguni sharti ainame. Pia wanasema, anayependa waridi, basi avumulie miiba. Vivyohivyo, hata katika tiba, wale wanaotaka uponyaji wamejikuta wakivumilia mambo mengi yanayoleta maumivu au kukera kama vile sindano na dawa. Hivyo, usishangae kuwa kuumwa na nyuki ikawa ni tiba tosha na thabiti kwako. Wanasayansi wa Chuo Kikuu cha Tiba cha Washington, Marekani wanaeleza kuwa, sumu ya nyuki inaweza kuponya maradhi mbalimbali ikiwamo kuharibu virusi vya Ukimwi bila kuharibu seli za mwili wa binadamu. Dk Joshua Hood, kiongozi wa utafiti huo anasema, ipo sumu kali iitwayo mellitin katika mwiba wa nyuki ambayo ina uwezo wa kuingia ndani ya mfuko unaozunguka kinga ya mwili wa binadamu na kuua virusi vya Ukimwi vilivyomo ndani.
Hata hivyo, imeelezwa kuwa sumu hiyo ya Mellitin iingiapo kwa wingi katika mwili wa binadamu, inaweza kuleta madhara.
Pia, Profesa Samule Wickline pia wa Marekani aliunda chembe ndogo zenye sumu ya mellitin, ambayo ina uwezo wa kuzuia saratani au dalili zozote z  vivimbe vya saratani.
Hapa nchini, Dk Augustine Godman mtaalamu wa magonjwa ya uzeeni na mshauri wa kisaikolojia anasema amejaribu kutumia tiba ya nyuki kwa wagonjwa 158 wenye matatizo kwenye viungio vya mwili (gouts), ambayo husababishwa na wingi wa tindikali ya uric katika damu.
Anasema dawa hiyo imeonyesha matokeo mazuri kwa wagonjwa wengi ambao hung’atwa na nyuki katika sehemu mbalimbali za miili yao. Dk Godman anasema, yeye humuweka mgonjwa nje ilipo mizinga ya nyuki na kisha kuwafungulia wadudu hao kutoka katika mizinga yao.
Anasema nyuki wana sumu ambayo inaingia katika mwili wa binadamu na kuondoa sumu iliyo mwilini.
Wakati huohuo, Dk Hood anasema kuwa, sumu ya nyuki ina uwezo mkubwa wa kutoa tiba na kuunda mafuta ya uke ambayo yanaweza kuzuia maambukizi ya VVU na kuviua virusi sugu.
Watafiti hao wanaeleza kuwa sumu ya nyuki ina uwezo wa kuua wale askari wakubwa wanaofanya mashambulizi katika kinga ya mwili.
nyuki
Profesa Ibadan Selako kutoka Chuo Kikuu cha Tiba Nigeria, anasema miba ya nyuki ndiyo silaha yao kuu wanayotumia wadudu hao kujilinda, kumlinda malkia na askari wengine, ni silaha ambayo ikitumiwa hata kwa binadamu inaweza kufanya maajabu.
“Mungu ameweka kitu cha ajabu katika sumu ya nyuki. Sumu hiyo inaweza kutibu mara tu nyuki anapokuuma na kuingiza miba yake katika mwili wako, baada ya dakika 45 au saa moja, nyuki hufa, na sumu aliyokuachia huingia katika mfumo wa mwili wako na kuanza kufanya maajabu,” anasema Profesa Selako.
Anasema, sumu ya nyuki inapoingia katika mwili wa mwanadamu husababisha maumivu na maumivu hayo pia huondoa maumivu. Salako anasema, ameshawahi kuwatibu watu wanaoishi na virusi vya Ukimwi na wengi wao wamepona kwa kutumia sumu hiyo ya nyuki.
Anasema mgonjwa huanza tiba ya kung’atwa na nyuki na huendelea na tiba hiyo kwa wiki nane hadi 12 kisha huenda kupimwa.
“Akienda kupima ataona kabisa kiwango cha virusi kwenye mwili wake kimepungua baada ya wiki nane hadi 12 za matibabu baada ya hapo tutaacha kumpa tiba, na kisha tutaendelea na tiba kwa wiki nyingine nne hadi tano, mgonjwa huenda kupima tena,” anasema
Profesa Selako anasema mgonjwa atakapokwenda kupima kwa mara ya pili, atagundua kuwa virusi katika mwili wake vinashuka kila anapoendelea na tiba na baadaye atakuta hana VVU. Anasema, nyuki wa kiume kwa kitaalamu huitwa ‘drone’ na hawana uwezo wa kutoa sumu kali kama nyuki wa kike ambao ndiyo malkia.
Shirika la Utafiti wa Ukimwi Duniani (FAIR) linasema duniani kote watu zaidi ya milioni 34 wanaishi na Virusi vya Ukimwi huku kati yao, 3.3 milioni wapo chini ya umri wa miaka 15. Wengine zaidi ya 7,000 hupata maambukizi mapya kila siku duniani.
Wakati huohuo, wanasayansi katika viwanda vya urembo duniani wamefanikiwa kutengeneza mafuta ya ngozi yenye sumu ya nyuki. Mafuta hayo ya ngozi huingia katika ngozi na kutoa sumu, kuirutubisha ngozi na kuondoa makunyanzi.
Mafuta hayo tayari yameshapata wateja  wengi, hasa baada ya Malkia Mtarajiwa, Kate Middleton kuyatumia kabla ya harusi yake na kuonyesha matokeo mazuri.
Kipodozi hicho kiitwacho Radial Bee Venom kina uwezo wa kuondoa ukavu usoni na makunyanzi na kinawasaidia zaidi watu wanaokaa katika jua kwa muda mrefu.
Dk Christopher Kim, Mkurugenzi  wa Taasisi ya Tiba ya Redbank anasema, tiba ya sumu ya nyuki iligunduliwa zaidi ya miaka 1,000 iliyopita na vielelezo vya tiba hiyo vinaonekana katika maandishi ya tiba za Ugiriki na Misri.
 Anasema tiba hiyo ilianza pindi wale wanaotunza nyuki walipoumwa mara kwa mara na wadudu hao kisha wakajisikia kupona baadhi ya maradhi kama maumivu ya kichwa, neva za fahamu, viungio vya mwili na kuwashwa.
 Kwa upande mwingine, zao la nyuki hawa yaani asali, ni tiba kwa vidonda, ngozi ya uso na huwasaidia watu wenye matatizo ya vidonda vya tumbo.
Dk Imelda Mwakitumbo wa Hospitali ya Mikocheni anasema asali ya nyuki hasa wadogo ina manufaa makubwa katika kuponya majeraha.
“Lakini pia mtu ambaye anataka kuondoa seli zilizokufa katika uso akipaka asali kwa maelekezo maalumu, anaweza kuipendezesha ngozi ya uso wake,” anasema Dk Mwakitumbo
Chanzo:Mwananch

Friday 29 November 2013

DAWA YA MAFUA ISIYO NA MADHARA

Watu wengi husumbuliwa sana na mafua makali na wakati mwingine kupiga chafya mfululizo. Ili kuondokana na tatizo la mafua unashauriwa kuandaa kinywaji kifuatacho kisicho na kemikali :
MAANDALIZI
Chukua :
1. Maji lita moja
2. Asali vijiko 3 vikubwa vya chakula
3. Tangawizi ya unga kijiko kimoja kikubwa cha chakula au tangawizi mbichi itwange upate mchanganyiko uliopondeka kijiko kimoja kilichojaa.
Chemsha mchangyanyiko wako wote huo kwa pamoja mpaka uchemke vizuri ambapo inategemea na moto wa jiko lako lakini mpaka utakapoona imechemka vizuri usiache ikakaukia jikoni inashauriwa dakika 15 hadi 20 inatosha.
Kisha iache ipoe na KUNYWA NUSU GLASI MARA TATU kwa siku yaani asubuhi , mchana na usiku.
mafua
Kwa wale walio na mafua sugu yanadondoka muda wote na kupiga chafya nyingi sana zisizo na idadi basi zitakata mara moja na siku ya pili zitaisha kabisa kumbuka kunywa dawa hii mwezi mzima au hadi miezi miwili utapona kabisa.
Kinywaji hiki ni dawa ya mafua safi kabisa unatumia siku moja tu unakua na nafuu kabisa ila dozi yake inataka utumie mwezi mmoja hadi mwezi mmoja na nusu mfululizo bila ya kuacha.

AFYA JE..?? FAHAMU KIUNDANI UGONJWA WA PUMU (ASTHMA) NA DALILI ZAKE...

Utangulizi Ugonjwa wa pumu ni ugonjwa sugu ambao huathiri njia za hewa ambazo huingiza na kutoa hewa katika mapafu. Upatapo ugonjwa wa pumu, kuta za ndani za njia ya hewa hupata maumivu (inflammation) na kuvimba. 

Maumivu katika njia za hewa huzifanya kujihami kwa kusinyaa na hivyo kupunguza kiasi cha hewa kinachopita kwenda kwenye mapafu. Hali hii husababisha muathirika kutoa mlio kama wa filimbi au mluzi wakati wa kupumua. 




Pumu husababishwa na nini? 

Bila shaka mpenzi msomaji umekua ukijiuliza swali hili mara kwa mara. Haifahamiki haswa ni sababu zipi zinazopelekea njia za hewa kupata maumivu na hivyo kupelekea mtu kupata pumu. 

Vyanzo mbali mbali vinaonyesha kuwa inatokana na mseto wa vitu kama tumbaku, maradhi na baadhi ya vizio

Pia kuna vitu katika mazingira ambavyo vinaweza kusababisha mtu kushambuliwa na pumu. Vitu kama vile mazoezi, vizio, viwasho (irritants) na maradhi yatokanayo na virusi. 

Baadhi ya vizio ni kama vifuatavyo: 

-Vumbi 
-Mende 
-Chavua (pollen) kutoka kwenye miti na majani 
-Magamba ya wanyama, manyoya n.k 

Viwasho kama: 
-Moshi wa sigara 
-Uchafuzi wa hewa 
-Harufu kali (kutoka kwenye rangi au chakula) 
-Msongo wa mawazo 
-Dawa kama Aspirin 
-Ugonjwa wa kucheua 
-Viwasho au vizio vitokanavyo na kemikali 
-Magonjwa ya njia ya hewa n.k.

Ieleweke kwamba orodha iliyotajwa hapo juu siyo kamilifu kwa maana kwamba haijasheheni vitu vyote vinavyoweza kuleta dalili za pumu na pia muathirika anaweza kuathirika na kimoja wapo au zaidi. 

Vigezo hatarishi 

Baadhi ya vigezo hatarishi vinavyoweza kuongeza uwezekano wa kusababisha ugonjwa wa pumu ni pamoja na: 

-Kuishi katika miji mikubwa, haswa katikati ya mji ambapo huongeza uwezekano wa kukutana na vizio 

-Kuvuta hewa iliyo na moshi 

-Kemikali zitokanazo na kilimo, dawa za kutengeneza nywele, rangi, vyuma, plastiki au vifaa vya elektroniki 

-Kuwa na mzazi mmoja au wawili wenye pumu 
-Kuathirika na maradhi ya mfumo wa hewa kama kikohozi na mafua wakati wa utoto. 

-Unene wa kupita kiasi (obesity) 

-Ugonjwa wa kucheua na kiungulia (Gastro esophageal reflux disease) 

Dalili za Pumu 

Baadhi ya dalili za kawaida za ugonjwa wa pumu ni kama zifuatazo: 

-Kikohozi: Mara nyingi kikohozi cha pumu huwa kikali nyakati za usiku au alfajiri na hivyo kumfanya mwathirika kutolala vizuri 

-Kutoa sauti ya mfano wa mtu anayepiga mluzi au filimbi wakati wa kupumua 

-Kifua kubana: Mgonjwa husikia kama kitu kinakandamiza kifuani au wakati mwingine husikia kama mtu amemkalia kifuani. 

-Kukosa hewa: Baadhi hujisikia kama hawawezi kupumua na kukosa hewa ya kutosha inayoingia au kutoka kwenye mapafu. 

-Kupumua haraka haraka 

Ikumbukwe kwamba si watu wote huwa na dalili zilizokwisha tajwa hapo juu na dalili zaweza kutofautiana kati ya mtu na mtu. 

Dalili pia zinatofautiana ukali. Wakati kwa mwingine dalili zinakuwa za wastani, wengine zinakuwa za kukera tu au mbaya kiasi cha kumzuia muathirika kufanya shughuli zake za kila siku. 

Vile vile wapo wengine ambao dalili zinakuwa mbaya kiasi cha kuhatarisha maisha. Dalili pia zaweza kutofautiana kwa kipindi zinapotokea. 

Wengine hupata dalili mara moja tu kwa mwezi, wengine kila wiki na wengine hupata dalili kila siku. Hata hivyo iwapo muathirika atapata matibabu sahihi anaweza kuishi na dalili chache au bila dalili kabisa


AFYA JE...?? UNAFAHAMU FAIDA ZA KULA MBEGU ZA MABOGA....?? SOMA HAPA NIKUJUZE...

Unaweza kuzidharau mbegu za maboga, lakini ni miongoni mwa mbegu zenye faida kubwa mwilini, zinazoweza kuzuia na kutibu hata magonjwa hatari yaliyoshindikana hospitalini.

 
Kwa mujibu wa utafiti wa kisayansi uliokwishafanyika, zifuatazo ni faida za kifya mtu anazoweza kuzipata kwa kula mbegu za maboga, zikiwa mbichi ama zilizokaangwa:

HUIMARISHA MOYO, MIFUPA
Mbegu za Maboga (Pumkin Seeds), zina kiwango kingi cha madini aina ya Magnesium ambayo ni muhimu kwa afya ya moyo, uimarishaji mifupa, mishipa ya damu na ufanisi wa utumbo mpana. Magnesium imeonesha uwezo mkubwa wa kuzuia mshituko wa moyo na kiharusi.

KINGA YA MWILI
Mbegu za maboga zina kiwango kingi cha madini aina ya Zinc, ambayo yana faida nyingi mwilini, zikiwemo uimarishaji wa kinga mwilini, ukuaji wa seli, macho na ngozi ya mwili. Vile vile Zinc huimarisha nguvu za kiume.

SARATANI YA KIBOFU
Kutokana na kuwa na kiwango kingi cha Zinc, utafiti umeonesha kuwa mafuta na mbegu zenyewe za mabogo huweza kutumika kama dawa ya kutibu saratani ya kibofu.

KINGA YA KISUKARI
Utafiti umeonesha pia kuwa mbegu za maboga huweza kuimarisha utokaji wa ‘insulin’ mwilini, hivyo kuwa kinga au kuleta ahueni kubwa kwa wagonjwa wa kisukari.

TIBA KWA WALIOFIKIA UKOMO
Mafuta ya mbegu za maboga hayana madhara, zaidi yana kirutubisho muhimu cha kurekebisha Cholesterol mwilini, kushusha shinikizo la damu, kuzuia uvimbe, maumivu ya kichwa, maumivu ya viungo vya mwili na vile vile huondoa maumivu mbalimbali yanayowapata wanawake wenye umri mkubwa waliofikia ukomo wa hedhi (Menopause).

UGONJWA WA INI
Mbegu za maboga pia zina kamba lishe na kinga kubwa ya kupambana na magonjwa nyemelezi. Mbali na hayo, mbegu zina virutubisho vinavyotoa kinga dhidi ya magonjwa ya ini na moyo.

USINGIZI
Kwa watu wenye matatizo ya usingizi, wanashauriwa kula punje kadhaa pamoja na tunda lolote muda mfupi kabla ya kupanda kitandani, utafiti umeonesha kuwa mbegu za maboga zina kirutubisho kinachochea uzalishaji wa homoni za usingizi kwa wingi.

UVIMBE
Mbegu za maboga zimeonesha kuwa na virutubisho vingi vyenye uwezo wa kuzuia magonjwa yote ya uvimbe mwilini, yakiwemo ya kuvimba miguu, vidole na hata majipu.

JINSI YA KULA MBEGU
Hakikisha unakula mbegu ambazo hazijaoza na zilizosafi ambazo hazijakaa muda mrefu. Kwa usalama zaidi, zioshe kwa maji safi kisha zianike, inapendeza zaidi ukila bila kukaanga, lakini pia ukiamua kula za kukaanga bado utapata faida zake, muhimu usiziunguze wakati wa kukaanga. Kwa kawaida hukaangwa kwa muda usiozidi dakika 10 tu.


KWA WANAWAKE: FAHAMU DALILI KUMI ZA AWALI ZA KUGUNDUA KAMA UNA UJAUZITO (MIMBA)...




MWANAMKE anapopata ujauzito kwa kawaida huwa anaanza kuona dalili ambazo si za kawaida. Na ni wakati huo ambao ni muafaka kwake kuanza kuuchunguza mwili wake.Maumivu kwenye matiti:

Hii ni dalili ya kawaida ya ujauzito ambapo nguvu za homoni mwilini huongezeka wakati yai linavyopata “rutuba”, jambo ambalo huongeza wingi wa damu na kuyafanya matiti ya mwanamke kuvimba na kuwa makubwa isivyo kawaida.

Maumivu mwilini:

Utaanza kusikia maumivu kama vile unataka kuingia katika siku zako. Kwa kawaida hali hii hutokea wakati yai likiwa linasafiri kwenda katika chumba cha mimba. Hivyo, hali hiyo husababisha sehemu hiyo itanuke taratibu na kusababisha maumivu hayo.

Kutokwa damu bila kutegemea:


"Wanawake wengi hufikiria kutokwa na damu kidogo ni dalili ya kuwa katika siku zao. Lakini, katika hali halisi, kutokwa damu kusikotegemewa, huwakumba asilimia 25 ya wanawake wakati wa kurutubika kwa yai,” anasema Goist. Ambaye anaendelea kusema kwamba iwapo utaona hedhi yako inakuwa fupi au inafanyika katika hali ambayo si ya kawaida, unashauriwa kwenda kufanya kipimo cha ujauzito..

Kuchoka:


Unapojisikia kuchoka na kukosa raha, au kutaka hata kulala wakati ukiwa kazini, lazima ufahamu kwamba mwili wako unajirekebisha kuingia katika kipindi kipya cha mabadiliko.

“Tambua kwamba katika kipindi cha mwanzo cha ujauzito ni muda ambao mtoto tumboni huanza kutumia sehemu ya nguvu zako na hivyo kukuletea uchovu na usingizi” anasema Goist.

Chuchu kuwa nyeusi:


Chuchu huanza kubadilika rangi yake kutokana na chembechembe za uhai (seli) kuanza kufanya kazi kwa nguvu zaidi. Hata hivyo, Goist anasema: “Wanawake wenye ngozi nyeusi hawawezi kuiona dalili hii mapema hadi muda wa kama wiki kumi zipite.”

Kichefuchefu:


Hali hii huwapata asilimia 85 ya wanawake wanapopatwa na ujauzito, ambapo nyakati za asubuhi ndipo hasa hujionyesha. 

Mwili kuvimba:


Kuna wakati kupungua kwa nguvu za uyeyushaji chakula kunaweza kukusababishia kuona tumbo limevimba na nguo zikawa zinakubana kutokana na chakula kujaa katika utumbo. Lakini hali hiyo ikiendelea na ukaona siku zako haziji, basi ni vyema ukatambua kwamba tayari una ujauzito na kinachokupasa ni kwenda kuhakikisha.

Kwenda haja ndogo mara kwa mara:


Kwenda haja ndogo kila mara ni dalili kwamba kibofu chako kimeanza kufanya kazi ya ziada, ambapo huwa kinafanya kazi ya kuondoa maji kwa uthabiti zaidi wakati wa ujauzito. Hali hii pia hujitokeza mwishoni mwa ujauzito, ambapo kibofu kitakapokuwa kinarudia hali yake ya kawaida baada ya kufanya kazi kwa muda mrefu.

Tamaa ya vitu mbalimbali:

Kutokana na mwili kuwa na “mzigo” wa ujauzito na hivyo kuchoka, hali hiyo humfanya mwanamke kutamani vitu mbalimbali ili kukidhi mabadiliko yaliyojitokeza katika mwili wake. Hii ni pamoja na kutaka vyakula fulani au kufanya mambo ambayo hapo nyuma alikuwa hayapendi.

Kuumwa kichwa:

Kuongezeka kwa damu kunaweza kusababisha kichwa kuuma japokuwa si sana, hususani katika wiki za mwanzo za ujauzito. Hata hivyo, hali hii hukoma mwili unapojirekebisha na mzunguko wa homoni unaotokana na ujauzito.

Kufunga choo:


Homoni ambazo husababisha mwili kuvimba pia husababisha kufunga choo kutokana na mfumo wa kuyeyusha chakula kutofanya kazi vyema. Hata hivyo hali hii inaweza kujitokeza zaidi wakati ujauzito unapoendelea kukua.

Kuwa na hasira


"Kutokana na kuongezeka kwa homoni za utendaji kazi mwilini, hali hiyo itakusababishia uchovu, na kukufanya kuwa na hasira,” anasema Goist

Kuongezeka kwa joto mwilini:


Kipimo cha joto la mdomo ni muhimu katika kutambua hali ya ujauzito. Kwa kawaida joto huongezeka kwa nyuzi moja au zaidi wakati yai likiwa linatunga mimba. Hali hiyo ikiendelea kwa zaidi ya wiki mbili, itakuwa inaonyesha dhahiri kwamba kuna “mtoto anakuja”.


MMMHHH HII KALI...!! MAITI HUFUKULIWA MAKABURINI ILI KUBADILISHWA NGUO KATIKA KISIWA CHA SULAWESI HUKO INDONESIA..

Image

Image 

KILA mwaka huko kaitika kisiwa cha Sulawesi, Tana Toraja, Indonesia, wafu (au maiti) hufukuliwa kutoka makaburini ili kubadilishwa nguo na kuwatembeza kijini hapo. Watu wa eneo hilo wa kabila la Toraja wana mila ya ajabu inayoiitwa Ma’nene  ambayo wanaamini mtu akifa bado yuko nao kwa hiyo inawalizimu kufanya mambo hayo kama kuwabadilisha nguo.

Wao mtu akifa hutakiwa kuzikwa katika eneo alilozaliwa na si lazima azikwe katika eneo alilofia.
Idadi kubwa ya watu wa eneo hilo ni Wakristo, wanaofuata ni Waislam na wengine ni Wapagani ambao wanajulikana kwa imani au madhehebu ya Aluk To Dolo yaani “Njia ya Mababu”.
Wao mtu akifa hutakiwa kuzikwa katika eneo alilozaliwa na si lazima azikwe katika eneo alilofia.
Idadi kubwa ya watu wa eneo hilo ni Wakristo, wanaofuata ni Waislam na wengine ni Wapagani ambao wanajulikana kwa imani au madhehebu ya Aluk To Dolo yaani “Njia ya Mababu”

MAMBO 10 YA KUFANYA KABLA HUJATIMIZA MIAKA 26...

1. Jifunze kuweka akiba ya fedha na iache bila kuigusagusa. 
2. Tafuta mpenzi sahihi na tulia naye, panga maisha. 
3. Ishi mahali pa peke yako, acha kuishi kwa wazazi au kupanga na nyumba na washkaji. 
4. Lipa madeni yako ya zamani. Yote! 
5. Tengeneza mwili ambao unataka halafu jitahidi kuu-maintain! Anza kuzingatia kuishi kwa kujali afya yako sana. 
6. Jitahidi uwe na marafiki ambao wana changamoto za kimaendeleo zitakazokusaidia.
 7. Anza kujinunulia assets kama ardhi na nyinginezo. 
8. Jifunze kuvaa vizuri na kwa heshima, si tu ilimradi umependeza. 
9. Kubali sasa kwamba umekua na acha tabia na mambo ya kitoto. 
10. Yaache ya zamani yapite na anza mapya.


UTAFITI: HAYA NDIO MADHARA YA INTERNET KWA VIJANA...SOMA HAPA KUYAFAHAMU...

 

MAMILIONI ya vijana duniani kote wanatumia intaneti, iwe nyumbani, shuleni, kwenye nyumba za marafiki au kwenye simu zao za mikononi.
Huenda watoto wako wanaielewa sana dunia ya intaneti kuliko wewe, na hata wanaweza kukuficha mambo wanayoyafanya kwenye intaneti.


Hata hivyo unaweza kujua mambo yanayowahangaisha vijana na watoto kwenye intaneti na si lazima uwe mtaalamu wa vifaa vya elektroniki ili uweze kumlinda mtoto wako.
Katika nchi zilizoendelea wakati fulani ilionekana kwamba ingekuwa salama kutumia intaneti ikiwa kompyuta ingekuwa mahali palipo wazi. Ilifikiriwa kwamba ukifanya hivyo haitakuwa rahisi kwa watoto na vijana kufungua vituo visivyofaa.

Bado wazo hilo linafaa kwa kuwa si jambo linalopatana na akili kuwaruhusu watoto kutumia intaneti katika chumba chao cha kulala. 

Jambo unaloweza kufanya 
Ukiwa mzazi au mlezi kuna mambo mawili ya hatari kuhusu intaneti ambayo yanahitaji mtu awe mwangalifu.
Wazazi hawawezi siku zote kuwazuia watoto wao kuendesha gari, lakini wanaweza kuhakikisha kwamba watoto wao wamefundishwa kuendesha gari kwa njia salama. Wazazi wengi wamechukua hatua kama hiyo kuhusu matumizi ya intaneti.

Michel ni mama anayeishi California, Marekani, ni mhasibu katika shule moja kubwa jimboni humo.
Anasema: “Kwa kawaida nimewatengea muda watoto wa kuangalia intaneti na ninaongea nao mara kwa mara kuhusu vituo visivyofaa na watu wanaoweza kukutana nao katika vituo mbalimbali wasio na nia nzuri kwao na pia madhara ya intaneti.”

Michel anasema ni jukumu la kila mzazi au mlezi kuhakikisha watoto wao hawafungui vituo visivyofaa na kuhakikisha wanawapa malezi mema na yenye maadili.
Wazazi ambao watoto wao wanatumia intaneti wanahitaji kujua mambo ya msingi kuhusu intaneti na watoto wao wanafanya nini wanapotuma ujumbe mfupi wanapofungua tovuti katika intaneti.

“Usikate kauli kwamba wewe ni mzee sana au huna elimu ya kutosha kujifunza,” anasema Marshay, mama mwenye watoto wawili, na kuongeza kuwa hutakiwi kuachwa nyuma na teknolojia.

“Watu wanaotoa huduma za intaneti na programu za kompyuta wametengeneza programu zinazoweza kuchuja au kuzuia ujumbe unaokuambia ufungue tovuti zisizofaa.
“Programu fulani zinaweza hata kumzuia mtoto asitoe habari za kibinafsi kama vile jina au anuani yake. Hata hivyo , mzazi anapaswa kujua kuwa vichujio hivyo havichuji habari zote mbaya. Pia, watoto wengine walio na ujuzi wa kompyuta wanaweza kujua jinsi ya kuepuka programu hizo,” anasema.

Huko Uingereza, asilimia 57 ya vijana walio na umri wa kati ya miaka 9 na 19 wanaotumia intaneti kila juma wamepata ponografia (picha za ngono), hata hivyo ni asilimia 16 tu ya wazazi wanaoamini kwamba mtoto wao ameona ponografia kwenye intaneti.

Wazazi wanapaswa kukumbuka kwamba vijana wengi wanaweza kutumia intaneti kupitia simu zao za mikononi. Simu za mikononi na intaneti licha ya kurahisisha wawasiliano pia zimekuwa ni kero, shuleni, kazini, nyumbani na sehemu nyingine muhimu.

Katika familia mbalimbali kazi za nyumbani zimekuwa zikifanyika kiuzembe na kuchelewesha muda wa chakula, hasa mwenye nyumba anapokuwa hayupo.

Nilipokuwa Morogoro mbali kabisa na mji, nilishuhudia katika familia moja msaidizi wa kazi za nyumbani jinsi anavyotumia muda mwingi kwa kusoma na kujibu ujumbe mfupi anaotumiwa.

Binti anayetarajia kujiunga na chuo kimojawapo hapa nchini anatumia muda mwingi kuwasiliana na marafiki, nilipompa kitabu cha kujisomea jibu lake lilinishtua alisema hivi: “Nimejaribu kusoma lakini sijaelewa chochote.” Akanirudishia kitabu.

Hao ni mfano mdogo sana kwa watoto wetu. Licha ya kuudhi wanafunzi katika vyuo mbalimbali hapa Tanzania wanapoteza muda wao mwingi sana kwa matumizi ya simu za mkononi na intaneti.
Uchunguzi uliofanywa Uingereza ulionesha kwamba kijana mmoja kati ya watano anaweza kutumia intaneti katika chumba chake cha kulala.

Lakini inaelezwa kwamba kuweka kompyuta mahali palipo wazi kunawasaidia wazazi kuchunguza kile ambacho watoto wao wanafanya kwenye intaneti na kuweza kuwatia moyo na kwafundisha wajiepushe na vituo visivyofaa.

Weka wakati ambao watoto wanaweza kutumia intaneti muda wanaopaswa kuitumia na vituo ambavyo hawapaswi kuvifungua.
Zungumzia sheria zako hizo pamoja na watoto wako, na uhakikishe kwamba wamezielewa na kuzifuata kwa manufaa yao na kwa wengine.

Bila shaka huwezi kuwachunguza watoto wako wasipokuwa nyumbani. Hivyo ni muhimu kuwafundisha kanuni zinazofaa ili wafanye maamuzi yenye heshima na hekima wakati ambao wewe uko mbali nao.

Wazazi wawaeleze watoto wao matokeo ya kuvunja sheria kuhusiana na intaneti na mambo mengine muhimu yatakayowasaidia maishani mwao.
Pia mzazi unapaswa kuchunguza jinsi watoto wake wanavyotumia intaneti na uwaeleze kwamba utakuwa unawachunguza. Kufanya hivyo si kuingilia faragha yao.
Kumbuka kwamba intaneti hutumiwa na watu wote. Shirika la Upelelezi la Marekani linapendekeza kwamba wazazi wanapaswa kuchunguza akaunti za watoto wao za intaneti, barua pepe zao na tovuti ambazo wanafungua.

Raymond Rugemalira Mwijage ni mwanasayansi na profesa anayeishi California, Marekani anasema: “Nyumbani kwangu nimetenga muda maalumu wa familia yangu kuangalia runinga na kufuatilia kwa ukaribu kila mwanafamilia anachofanya kwenye intaneti.”

Anasema huwezi kuchunguza jinsi mtoto wako anavyotumia intaneti kila wakati. Hivyo, ni viwango unavyofundisha na mifano unayotoa ndivyo vitawalinda watoto wako zaidi.
Mwijage anasema tenga wakati wa kuzungumza na watoto wako kuhusu hatari za intaneti.

Njia bora zaidi za kuwalinda watoto wako dhidi ya hatari za intaneti ni kuwasiliana nao waziwazi.
Anasema: “Tulizungumza na wavulana wetu kuhusu watu wabaya kwenye intaneti. Pia tuliwaeleza ponografi ni nini, kwa nini wanapaswa kuiepuka na kwa nini hawapaswi kamwe kuwasiliana na watu wasiowajua.
“Intaneti imekuwa pia ikipotezea watu muda wa kufanya kazi. Nilipokuwa namuuguza ndugu yangu katika hospitali moja kubwa (jina limehifadhiwa) jijini Dar es Salaam nchini Tanzania, jopo la madaktari limemzunguka mgonjwa, cha kushangaza mmoja wao hana muda na kinachoendelea, yuko ‘busy’ na simu yake ya mkononi akichati.”

Madhara ya simu za mkononi yameathiri sana sekta ya elimu kwa nchi nyingi duniani.
Inasikitisha sana nchi zinazoendelea zimekuwa wahanga wakubwa wa janga hili; nilipokuwa mkoani Morogoro (vijijini ) Tanzania kwa tafiti, ikiwamo elimu, nilichokabiliana nacho cha kutisha ni simu za mkononi, runinga na tamthilia ni moja ya mambo makuu yanayosababisha kushuka kwa kiwango cha elimu.

Unaweza kuwalinda watoto
Jitihada zinahitajika ili kuwalinda watoto wako kutokana na hatari za intaneti na njia ya kupata habari kupitia vifaa vya elektroniki inabadilika kila mara.
Huenda pia teknolojia mpya ikawa na faida na hatari nyingi sana kwa watoto.

Wazazi wanaweza kuwaandaa watoto wao kwa ajili ya hatari watakazokabiliana nazo wakati ujao.
Hekima ni ulinzi kama vile pesa ni ulinzi pia. Wasaidie watoto wako kuwa na hekima ili waweze kupambanua zuri na baya.

Pia wasaidie waelewe jinsi ya kuepukana na hatari za intaneti na jinsi ya kuitumia kwa njia inayofaa.
Kwa namna hii, intaneti inaweza kuwa kifaa kizuri ambacho hakitahatarisha usalama wa watoto wako.
Wataalamu wanaamini kwamba huenda kila siku zaidi ya watu 750,000 wanaovizia watoto ili wawarubuni kufanya nao ngono wanatumia vituo vya maongezi na vituo vya kuwatafutia watu wachumba.

Marekani, zaidi ya asilimia 93 ya vijana wenye umri wa kati ya miaka 12 na 17 wanatumia intaneti.
Katika nchi zinazoendelea, intaneti imegeuka pia kuwa kero na kuathiri maendeleo mazuri kimasomo na maisha ya vijana, watoto na watu wazima kwa ujumla.


Mpasuko Chadema sasa Baraza kuu

BAADA ya Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Willibrod Slaa kufunga mjadala wa mgogoro unaoendelea ndani ya chama hicho, agizo hilo limeonekana kufuatwa vema na wajumbe wa Kamati Kuu, lakini limewafungua wajumbe wa Baraza Kuu, Mkutano Mkuu na taasisi za chama hicho.
Tayari imeripotiwa kuwa uamuzi wa chama hicho kumvua madaraka aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu, Kabwe Zitto na aliyekuwa mjumbe wa Kamati Kuu, Dk Kitila Mkumbo, umeipasua Kamati hiyo katika vipande vya wafuasi wa wagombea uenyekiti wa chama hicho katika uchaguzi ujao, Mwenyekiti wa sasa Taifa, Freeman Mbowe na Zitto.
slaa22
Miongoni mwa wajumbe wa Kamati Kuu wanaotajwa kumwunga mkono Mbowe ni Dk Slaa, Mwanasheria Mkuu wa Chama hicho, Tundu Lissu, Msemaji wa Chama hicho, John Mnyika na Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema.
Waliojitokeza waziwazi kumwunga mkono Zitto ni Dk Mkumbo, aliyekuwa Mwenyekiti wa Mkoa wa Arusha, Samson Mwigamba ambao kwa hatua hiyo wamevuliwa nyadhifa zao na aliyekuwa Mwanasheria wa Mbowe, Albert Msando ambaye sasa ni Mwanasheria wa akina Zitto.
Wengine wanaotajwa kumwunga mkono Zitto ni aliyekuwa Makamu Mwenyekiti , Said Arfi ambaye uamuzi wa kumvua Zitto madaraka, ulisababisha ajiuzulu nafasi hiyo.
Hata hivyo, Profesa Mwesiga Baregu, ameripotiwa kukionya chama kwa hatua hiyo, akisisitiza kuwa baada ya uamuzi huo wa Kamati Kuu dhidi ya Zitto, chama kilitakiwa kisubiri baraka za Baraza Kuu, ndipo uamuzi huo utangazwe.
Wafuasi Baraza Kuu Jana Mwenyekiti wa Chadema wa Wilaya ya Temeke na mjumbe wa Baraza Kuu, Patrick Joseph, alitoa kauli iliyodhihirisha kuwa yeye ni mmoja wa wanaomwunga mkono Zitto.
Joseph katika kauli yake, alionekana kuungana na Katibu wa Chadema wa Mkoa wa Geita, Abdalah Hamis, ambaye hakumung’unya maneno, kwani aliweka wazi kuwa yeye atamwunga mkono Zitto. Mwenyekiti huyo wa Temeke, aliitisha mkutano na waandishi wa habari akimtaka Mbowe, kuitisha mkutano wa dharura wa Baraza Kuu, ili litoe uamuzi sahihi kuhusu Zitto na wenzake.
Pamoja na kuwa yeye si mjumbe wa Sekretarieti ya chama, inayopanga ajenda za Baraza Kuu, Joseph alisema ajenda ya kikao cha Baraza hilo, ni kutaka viongozi wawaeleze wajumbe kwa nini wamesambaza waraka wanaodhani unawadhalilisha Zitto, Dk Mkumbo na Mwigamba, wakati waraka huo umekidhalilisha chama kwa kuonesha udhaifu wa Mwenyekiti na Katibu Mkuu.
Akionekana kuwasemea wajumbe wenzake wa Baraza hilo, Joseph alisema katika mkutano huo, wajumbe watataka waelezwe kwa nini wasiamini kwamba uamuzi huo umeathiriwa na hofu ya uchaguzi wa ndani wa chama.
Pia watataka sababu zilizoifanya Sekretarieti ya Kamati Kuu, itangaze ratiba ya uchaguzi mkuu wa ndani, baada ya kuwachafua miongoni mwa watu waliotarajiwa kugombea nafasi, mpaka kuwavua uanachama.
Mjumbe huyo bila kuonesha hofu ya kuvuliwa madaraka kama wenzake walivyofanyiwa, alisema umefika wakati wa kuijenga Chadema bila kufuata masuala ya ubaguzi wa kidini, kikabila ama kikanda kama ambavyo inajulikana nje. Akifafanua hoja hiyo ya ubaguzi, alisema kuwapo kwa Zitto na Arfi katika nafasi za viongozi wa kitaifa, ilikuwa ni ishara ya kutokuwa na udini ndani ya chama.
“Sasa inawezaje kuwatimua na kuwaita wasaliti watu ambao mmekuwa mkijivunia kuwa ni ishara kwamba hakuna udini?”
Alihoji Mwenyekiti huyo wa Chadema Temeke, na kusisitiza kuwa hayuko tayari kuburuzwa wala kuruhusu baadhi ya viongozi waendelee kuibomoa demokrasia wanayoitangaza kila kukicha.
Joseph alisema chama chao kimekuwa na tabia ya kuingia kwenye migogoro kila kinapokaribia kwenye uchaguzi wa ndani hali inayosababisha kuchafuana na kutukanana miongoni mwa viongozi kwa kuitana wahaini na wasaliti.
Alisema amefadhaishwa na uamuzi wa Kamati Kuu dhidi ya Zitto na Dk Mkumbo, kwani haikuwa na mamlaka ya kikanuni wala kikatiba kufanya hivyo na kuutangaza kwa umma.
Kauli hiyo ya Joseph, ilitolewa pia na Dk Mkumbo, Msando ambaye pia ni Mjumbe wa Mkutano Mkuu na Profesa Baregu. Hata hivyo, imekuwa ikipingwa na Lissu kwa kutumia Katiba hiyo hiyo ya Chadema, kwamba kuna kipengele kiliongezwa katika Katiba ya sasa, kinachoruhusu Kamati Kuu kuchukua uamuzi kama huo inapoona inafaa.
Joseph alisisitiza kuwa haingii akilini chama kinachopanga mikakati ya kushika Dola, kifukuze na kuogopa watu wanaopanga mikakati ya wao kushinda uchaguzi ndani ya chama.
“Kama ni kweli kupanga mikakati ya uchaguzi ndani ya chama ni uhaini na usaliti, basi operesheni zetu za chama ikiwemo ya M4C zenyewe zinapaswa kuwa uhaini uliopitiliza kwa kuwa nayo ni mikakati ya chama kushika Dola,” alisema Patrick. Mikoani Juzi Katibu wa Mkoa wa Geita, Hamis alitamka:
“Nikiwa Katibu wa Chadema, Mkoa wa Geita nasema mimi na wenzangu pia wote ndani ya mkoa wetu tutakuwa nyuma ya Zitto. Nyakati za uonevu, manung’uniko na kubaguliwa sababu tu za eneo, ukanda, udini na kuchaguliana marafiki zimekwisha.”
Katibu wa Chadema wa Wilaya ya Tanga, Harid Rashid, ambaye alifuatana na mjumbe wa Mkutano Mkuu Taifa, Hussein Baruti na mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya Wilaya ya Tanga, Mohamed Aufi, aliripotiwa kusema hakubaliani na uamuzi wa Kamati Kuu.
Rashid alisema Kamati Kuu ilikuwa na njia nyingi za kulipatia ufumbuzi jambo hilo badala ya kuwavua uongozi. Alisema wameamua kuwa wazi kuhusu tukio hilo kutokana na ukweli kuwa Zitto ni mtu muhimu katika uongozi wa chama.
Kundi la vijana wanaodaiwa kuwa wafuasi wa Zitto jijini Mbeya nao wanadaiwa kurushiana makonde na viongozi wa Chadema katika ofisi ya chama hicho Mbeya Mjini kwa madai ya kutofautiana misimamo kuhusu uamuzi wa Kamati Kuu. Mwenyekiti wa Chadema wa Wilaya ya Mbeya Mjini, David Mwambigija ‘Mzee wa Upako’, alithibitisha kutokea kwa vurugu hizo juzi mchana.
Mjadala wafungwa Kudhihirisha kuwa wajumbe wa Kamati Kuu wametii agizo la Dk Slaa la kufunga mjadala huo, jana gazeti hili lilipotafuta namna ya kumpata Mwigamba, alikuwa akikata simu zake.
Lilipomtafuta Profesa Baregu, alipokea lakini alijibu kwa ufupi kwamba kwa sasa hawezi kuzungumzia mambo ya Chadema. Wafuasi wa Mbowe Baada ya Zitto na Dk Mkumbo kuzungumza baada kuvuliwa madaraka, Mnyika na Lissu waliitisha mkutano na waandishi wa habari kukanusha yote yaliyozungumzwa.
Katika mkutano wao akina Mnyika, walidai kuwa waraka uliochapishwa na magazeti kuwa ndio uliomponza Zitto kwa kuwa si uliowasilishwa mbele ya Kamati Kuu.
Lakini mwandishi wa waraka huo, Mwigamba alijibu haraka kuwa hakuna kilichohaririwa bali waraka huo ndio sahihi. Kutokana na vurugu zilizotokea Kigoma, wafuasi wa Mbowe walisema ni za kutengeneza na leo wamejipanga kufanya mkutano kutetea hoja kuwa Kigoma anakotoka Zitto, wanaunga mkono uamuzi wa Kamati Kuu.
Mbali na kikao hicho cha Kigoma, pia Mratibu Mkuu wa Umoja wa Wanafunzi wa Vyuo Vikuu (Chasso), Dar es Salaam, Elihuruma Himida, alisema leo umoja huo utatoa kauli kupinga matamko ya wanaojiita wanafunzi wa vyuo vikuu, waliosema watazunguka nchi nzima kumwunga mkono Zitto.
Elihuruma pia alidai kuwa mkutano wa Zitto kujibu hoja za kuvuliwa madaraka, uliandaliwa na wanachama wa Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM), akina Juliana Shonza, waliohudhuria mkutano huo wa Zitto, huku viongozi wa Baraza la Vijana la Chadema (Bavicha), wakizuiwa kumsikiliza kiongozi huyo.
Source:Habarileo

Hivi Ndivyo DIANOND Alivyowafanyia Usaili Waliotuma maombi ya Kujiunga kundi lake la WCB-WASAFI..




Siku ya jana tulifanya zoezi la kuwafanyia interview
 baadhi ya watu waliotuma maombi yao kwa
 mujibu wa ,tangazo la kazi nilillolitoa
                                                                      juzi,mwitikio
 wa watu ulikuwa mkubwa,watu waliotuma
 email zao pamoja simu,kiasi ilituwia vigumu 
kuwataka wote waje kwenye interview,ilitubidi
 tuchague baadhi ya watu ambao tulihisi wanaweza
 kukidhi sifa tulizozihitaji ingawa nao pia tulipata
 changamoto ya wengi wao kuja pasipo kuzingatia maelekezo 
 na maagizo ya tangazo lilivyotaka,hivyo jana 
nikishilikiana na wataalamu wa hizo sekta tulisaili
 na mwisho wa siku tutachukua wale wenye viwango
 tunavyovihitaji na kuungana na team ya WCB-WASAFI,.....
Ahsanteni sana

WATANZANIA WAWILI WANASWA NA SHEHENA YA KILO 55 ZA MADAWA YA KULEVYA HUKO AFRIKA KUSINI...!!



Johannesburg/Dar. 
 Watanzania wawili wanahojiwa na Polisi wa Afrika Kusini baada ya kukamatwa jana na kilo 55 za dawa za kulevya. 


Watu hao wawili wanatazamiwa kufikishwa mahakamani kesho kujibu tuhuma za kukamatwa na dawa hizo zenye thamani ya Rand75 milioni (Sh11.7 bilioni).

Maofisa wa Kikosi Maalumu cha Kupambana na Makosa ya Jinai na Rushwa cha Afrika Kusini (The Hawks), kiliwakamata watu hao katika Kitongoji cha Kempton Park, Ekurhuleni, Jimbo la Gauteng.

Msemaji wa Hawks, Paul Ramaloko alisema jana kuwa maofisa hao walivamia nyumba waliyokuwa wanaishi Watanzania hao na kukuta mzigo huo.

Hata hivyo, alikataa kutaja majina ya watu hao kwa kuhofia kuharibu uchunguzi akisema bado walikuwa wanawasaka watuhumiwa zaidi wakiwamo raia wa Afrika Kusini.

Alisema kikosi chao kimepata mafanikio makubwa kwa kukamata dawa nyingi kiasi hicho... “Tunakaribia kuwakamata vinara wa biashara hiyo, maana tumeelezwa kuna kundi kubwa la watu wazito,” alisema Ramaloko. Hii inakuwa mara ya pili katika kipindi cha miezi minne kwa Watanzania kutuhumiwa kubeba dawa hizo.

Julai mwaka huu, wasanii wawili Agness Gerald `Masogange’ na Melissa Edward walikamatwa kwenye Uwanja wa Ndege wa Oliver Tambo, Johannesburg wakiwa na kilo 180 za kemikali aina ya ephedrine zenye thamani ya Sh7 bilioni.

Baada ya kukaa miezi miwili jela, Masogange alipatikana na hatia ya kuingiza kemikali hiyo, ambayo hutumika kutengeneza dawa za kulevya na kutozwa faini ya Rand 15,000 (Sh2.3 milioni).

Melissa aliachiwa huru baada ya kuonekana hana hatia.

Wasafirishaji sasa watumia samaki

Katika hatua nyingine, wasafirishaji wa dawa za kulevya inasemekana wamebuni mbinu mpya ya kutumia samaki kusafirisha bidhaa hiyo haramu.

Akizungumza jana wakati wa uteketezaji wa dawa za kulevya, Mkuu wa Kitengo cha Kudhibiti Dawa za Kulevya, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP), Godfrey Nzowa alisema wanatumia samaki kwa kuwa wana harufu kali.

----Mwananchi